• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA DAWA KATIKA VITUO VYA AFYA.

Posted on: March 28th, 2023

Imeelezwa kuwa Serikali itaendelea kutafuta njia za kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vyote vya Afya vilivyopo hapa nchini.

Hayo yamebainishwa Machi 27 mwaka huu na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Tawala na Rasilimali Watu Bw. Herman Tesha wakati akifungua mafunzo ya mfumo wa Shitiri yaliyofanyika katika Hoteli ya Glonency iliyopo Katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Katibu Tawala huyo amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha upatikanaji wa vifaa tiba na dawa unafikia asilimia 100 katika vituo vyote kuanzia ngazi ya Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya na Mikoa hapa nchini, hivyo umeanzisha mfumo huo wa mshitiri kwa lengo la kuhakikisha hali ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba unafikia asilimia 100 na kuondoa changamoto ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya.

Amesema kupitia mfumo huo wa Mshitiri ambao Serikali imeuanzisha, utasaidia kuongeza upatikanaji wa vifaa tiba na dawa kutoka kwa mashirika binafsi yanayotambulika na Serikali ili kuifikia asilimia 100 inayotakiwa baada ya MSD kushindwa kufikia asilimia hizo.

Aidha, Bw. Tesha amewataka watendaji wa Halmashauri kusimamia ukusanyaji wa mapato katika vituo vya afya ili kufikia lengo la asilimia 100 kwa kuwa mapato hayo ndiyo yatakayo fanikisha upatikanaji wa vifaa tiba hivyo pamoja na dawa.

Kwa upande wake mwezeshaji wa Kitaifa wa mfumo huo Dkt. Abdilah Njopeka amesema lengo la mafunzo hayo ni kutawanya mwongozo wa utekelezaji wa mfumo huo ili kuongeza ufanisi katika upatikanaji wa dawa.

Nae Bi. Fiona Chilunda Mshauri Mwandamizi wa masuala ya dawa na vifaa tiba kutoka mradi wa HPSS amesema wataendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha kuwa dawa na vifaa tiba vinapatikana kwa asilimia 100, ameongeza kuwa mfumo huo utafanya kazi pale ambapo MSD ikishindwa kutekeleza mahitaji ya vituo vya afya kwa asilimia hizo 100.

Dkt. Mariam Bendera akimuwakilisha Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro ameishukuru Serikali kwa kuwaletea mafunzo ya mfumo huo ambao utawasaidia kuongeza ufanisi katika utendaji na uendeshaji wa vituo vya afya kwa kuwa hali ya upatikanaji wa vifaa tiba na dawa utaimarika Zaidi kupitia mfumo huo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha utekelezaji wa Mfumo huo wa Mshitiri ambao ulizinduliwa Dodoma hivi karibuni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Angellah Kairuki kwa kushirikiana na Wizara ya Afya.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.