• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUENDELEA KUTOA MIKOPO YA RIBA NAFUU.

Posted on: December 5th, 2024



Serikali Mkoani Morogoro imesema itaendelea kushirikiana na Vijana kwa kutoa  fursa za mikopo yenye riba nafuu kwa vikundi mbalimbali vikiwemo vikundi vya wajasiliamali, watu wenye ulemavu na wabunifu ili kujikwamua na hali duni ya maisha.

Kauli hiyo imebainishwa Disemba 5, 2024 na Afisa Maendeleo ya vijana Mkoa wa Morogoro Bi. Mariana Lutananurwa wakati akifungua Kongamano la siku moja la vijana  lililojumuisha vijana kutoka mataifa mbalimbali yakiwemo Uingereza, Uganda na Tanzania lililofanyika ukumbi wa mikutano wa Chuo kikuu cha Jordan mjini Morogoro .

Akifungua kongamano hilo lililolenga kuwakutanisha vijana wanaojitolea katika sekta binafsi na sekta za umma ili kutoa elimu, kupeana uzoefu na kujaddili mikakati ya namna vijana kushiriki kwenye maendeleo endelevu, Bi. Mariam Lutananurwa ametumia fursa hiyo kuwaahidi vijana hao kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na wenye Ulemavu itaendelea kutoa mikopo yenye riba nafuu kupitia Halmashauri zake.

Kwa sababu hiyo Bi. Mariana amesema pamoja na shughuli za kujikwamua kimaisha bado Vijana wanao wajibu wa kujikwamua na umaskini huo kwa kuwajibika kuimarisha amani, mshikamano na kutunza maadili ya Taifa.

"....kama vijana tunaowajibu wa kujikwamua na umaskini kwa kuwajibika kuimarisha amani, upendo na mshikamano..." amesema Bi. Mariana Lutananurwa.

Akizungumzia shirika la Kijana Initiative Organisation (KIO) ambalo limeratibu kongamano hilo Bi. Mariana amesema shirika hilo limekuja na mpango mkakati wa kuhakikisha vijana wanajikwamua kiuchumi kwa kutoa elimu kupitia wawezeshaji wanaofanya kazi sehemu mbalimbali duniani hivyo amewataka vijana watumie vema fursa hiyo.

Aidha, Bi. Mariana amesema shirika hilo linajihusisha kusaidia vijana hususan wajasiriamali kwa kuwajengea uwezo, kutoa fursa za elimu kwa vijana (scholarship), elimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi hasa utunzaji wa mazingira na elimu kuhusu matumizi ya mitandao bila kuathiri tamaduni, mila na desturi.

Kupitia shirika la KIO, amesema vijana wataweza kupaza sauti katika kukataa viashiria vya ukatili wa kijinsia, biashara haramu zinaazotokana na mabadiliko ya teknolojia ambayo inaharibu mila na desturi zilizopo huku akiahidi kuwa Mkoa huo utatoa ushirikiano  kwa shirika la KIO na kuhakikisha vijana wananufaika na maarifa yatakayotolewa na shirika hilo.

Klwa upande wake, Mkurugenzi wa KIO Bi. Rose Mmbaga amesema shirika hilo limelenga kuwaunganiasha vijana, kuwapa taarifa na kuwahamasisha ili kuweza kuchangia maendeleo endelevu katika jamii na kwamba litawasaidia vijana kupata mawazo mapya kupitia majadiliano na kuweza kuibua changamoto zinazowakabili na kuzitafutia majibu.

Naye, Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Jordan  Bw. Alimia Libela amewashauri vijana kuwa na mitazamo ya kugundua fursa yenye tija ili kuendelea kuisaidia jamii inayowazunguka na kuepuka kuilalamikia  serikali kuhusu ajira.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.