• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali kuendeleza Vita Dhidi ya UKIMWI.

Posted on: December 1st, 2021

Serikali kuendeleza vita dhidi ya UKIMWI.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Martine Shigela amesema Serikali ya Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan itaendeleza mapambano  dhidi ya maambukizi ya Virus vya UKIMWI na magonjwa mengine ya mlipuko kwa kushirikiana na wadau mbalimbali lengo likiwa ni kupunguza ama kutokomeza kabisa maambukizi ya magonjwa hayo.

Shigela ameyasema hayo Disemba Mosi mwaka huu wakati wa Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ambayo huadhimishwa Disemba Mosi kila mwaka ambapo mwaka huu Kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Ofisi ya Kata ya Mazimbu katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Shigela amesema kuwa, katika kuendeleza mapambano hayo, Serikali imekuwa ikiboresha miundombinu ya sekta ya Afya kwa kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kusaidia vita dhidi ya UKIMWI  na magonjwa mengine kwa kuboresha huduma za afya ili ndugu zetu walioathirika na ugonjwa huo waweze kupata dawa bila malipo ili kupunguza makali ya virusi hivyo.

Aidha, amesema Serikali imeendelea na jitihada za utoaji wa elimu kwa jamii kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi hayo na pia jamii kuwa na utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara kwa lengo la kujua mwenendo wa afya zao.

 “…..Serikali inaendelea kutoa huduma bure za matibatu dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi, yote hayo ni mikakati ya serikali ya kuonesha dhamira iliyo nayo, na hasa hasa serikali ya awamu ya sita imekuja na kasi Zaidi ya kuhakikisha mapambano dhidi ya Ukimwi yanaendelea”.

Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa, serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030 maambukizi ya virusi vya UKIMWI yanapungua ama kutokomezwa kabisa hadi kufikia asilimia sifuri huku akiwataka watanzania  kuendelea kuchukua taadhari dhidi ya mlipuko wa UVIKO 19 kwa kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu wa afya.



Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando amesema kuwa maambukizi ya VIRUS vya ugonjwa wa UKIMWI kwa sasa yameongezeka hadi asilimia  4.2 kutokana na wimbi la ongezeko la vijana kunzia umri wa miaka 15 na kuendelea, hivyo serikali ya Mkoa imeelekeza nguvu zake katika kuhakikisha kuwa maambukizi yanapungua kwa kutoa elimu kwa jamii kuchukua taadhari na kutoa huduma kwa waathirika wa UKMWI.

Nae Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio, pamoja na kuzungumzia ugonjwa wa UKIMWI kuwa ndani ya kipindi cha miaka 17 maambukizi Mkoani humo yameongezeka kwa asilimia 4.2, amezungumzia  hali ya ugonjwa wa UVIKO 19 kuwa mpaka sasa ni watu elfu 46 pekee kwa awamu ya kwanza ndio waliojitokeza kupata chanjo ya ugonjwa huo, hivyo kutoa wito wananchi kuendelee kujitokeza kupata chanjo.


Nae shuhuda wa watu wanoishi na virusi vya UKIMWI Bi. Anna William ambae pia ni makamu mwenyekiti wa Baraza la Konga, ametoa ushuhuda mbele ya Mkuu wa Mkoa kupata maambukizi hayo tangu mwaka 2005 hadi sasa  hajatetereka kimaisha kwa kuwa mara alipojigundua ana maambukizi hayo alianza kutumia dawa za ARV, hivyo amewataka watanzania kwenda kupima afya zao mara kwa mara, na kuepuka ngono nzembe ili kupunguza maambukizi hayo.

Maadhimisho  hayo ya siku ya UKIMWI duniani kwa mwaka huu yana kauli mbiu isemayo ”Zingatia Usawa, Tokomeza UKIMWI, Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko”

 

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.