• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali kuhakikisha upatikanaji wa umeme kuvutia wawekezaji nchini.

Posted on: August 5th, 2024


Serikali hapa nchini imesema inaweka mipango na mikakati ya kusimamia upatikanaji wa  umeme wa kutosha katika maeneo ya Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi  ili kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kuja kuwekeza na  kujenga viwanda mbalimbali kwa maendeleo ya watanzania.

Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amebainisha hayo leo Agosti 5, 2024 wakati wa Mkutano wa hadhara katika Mji mdogo wa Ifakara na kuongea na wananchi wa Wilaya za Ulanga, Malinyi na Kilombero katika viwanja vya CCM vilivyopo Mjini Ifakara.

Dkt. Samia amesema ili kuongeza thamani ya viwanda hapa nchini ni lazima nishati ya umeme iwepo ya kutosha  ili kuvutia wawekezaji kuja kwa wingi  kujenga viwanda na kuongeza thamani ya mazao kwa maendeleo ya Wilaya hizo na Taifa kwa ujumla.

"... Niwahakikishie kwamba Serikali itasimamia kuwa na umeme wa uhakika katika maeneo haya na kufanya uwekezaji uwe mkubwa zaidi na kuleta maendeleo kwa watu wa Kilombero, Ulanga na Malinyi.." amesisitiza Dkt. Samia .

Aidha Dkt. Samia amesema kupitia Wakala wa Usambazaji wa Umeme Vijijini (REA) wameweza kusambaza umeme kwa vijiji 110 vya Wilaya ya Kilombero na kazi iliyobaki ni kusambaza nishati hiyo kwenye vitongoji na kuunganisha kwenye taasisi na kwa wananchi.

Aidha Dkt. Samia amesema, Serikali inatumia gharama kubwa kujenga  miundombinu ya Elimu  ikiwemo ujenzi wa madarasa pamoja na shule za ufundi ili kuwawekea mazingira mazuri vijana wapate elimu, hivyo ametoa wito kwa wazazi hapa nchini kuwapeleka watoto shule kwa lengo la kupata maarifa na ujuzi utakao wasaidia katika kujiajiri na kuajiriwa katika viwanda mbalimbali.

Katika hatua nyingine Dkt. Samia ameagiza viongozi wa Serikali ngazi ya wilaya na Mkoa wa Morogoro kusimamia wakulima wa zao la mpunga wauze kwa bei ya faida ili kukuza uchumi wao badala ya kuuza mazao yao kwa hasara ikiwemo kuuza mpunga kwa kutumia mfumo wa lumbesa jambo ambalo amelikemea.

Sanjari na hayo Dkt. Samia amesema Serikali inampango wa kulifanya bonde la Kilombero kuwa bonde la umwagiliaji ambapo wataanza  ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhia maji yanayoingia kwenye bonde hilo, maji hayo yataifadhiwa wakati wa mvua na wakati wa kiangazi wakulima watayatumia kwa ajili ya umwagiliaji, hivyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kukamilisha mradi huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.