• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

Posted on: April 25th, 2025

SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko mbioni kujenga barabara ya Lupiro hadi Malinyi kwa kiwango cha lami ili kuwaondole adha wananchi wa Wilaya ya Ulanga na Malinyi ambao hukumbana na changamoto hizo kila mwaka katika sekta ya usafiri na usafirishaji.

Kauli hiyo ya serikali imebainishwa Aprili, 24, 2025 na Waziri mwenye dhamana ya Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega alipotembelea Wilaya za Kilombero na Malinyi Aprili 24, 2025 baada ya kujulishwa uwepo wa uharibifu mkubwa wa madaraja kusombwa na maji na baadhi ya barabara za Wilaya hizo kuharibiwa na Mvua zinazoendelea kunyesha sasa.

Waziri huyo wa Ujenzi aliyeambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Alhaji Adam Kighoma Malima waliwasili katika Wilaya hizo wakitokea Mkoani Dodoma kwa njia ya Helkopta na kutembelea maeneo yaliyoharibiwa.

Akiwa Wilayani Malinyi, Waziri Ulega amewaambia wananchi wa Wilaya hiyo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa shilingi Bil. 18 kwa ajili ya kujenga madaraja mawili, ya Mto Fulua na daraja la mto uliopo Kijiji cha Iragua ambayo ni korofi na huleta adha kwa wananchi wa Wilaya hizo.

“Rais samia ameniambia kwamba haya madaraja yalikatika toka mwaka jana Rais amekupeni pesa shilingi Bilioni 18  hizo ni za madaraja peke yake ”

Aidha, Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega amebainisha mbele ya wananchi hao kuwa Rais Samia Suluhu Hassan pia ameridhia ujenzi wa Barabara ya kutoka Lupilo Wilayani Ulanga hadi Malinyi kwa kiwango cha lami yenye urefu wa zaidi ya km.100 itakayojengwa kwa bajeti ya mwaka 2025/2026.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Alhaji Adam Kighoma Malima awali alimuomba Waziri wa Ujenzi kupata ufumbuzi wa kudumu wa madaraja ambayo husombwa na maji kila mwaka na kusababisha changamoto ya usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Wilaya za Malinyi na Ulanga. 


MWISHO                                                         

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.