• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali kuuza tani 148,000 za asali nje ya nchi.

Posted on: August 5th, 2023

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) amesema mwaka huu Serikali imepanga kuuza nje ya nchi  tani 148,000 za asali hivyo amewataka wafugaji wa nyuki kuzalisha asali hiyo wa wingi ili kutimiza lengo hilo.

Waziri Mchengerwa ameyasema hayo Agosti 4 mwaka huu alipotembelea banda la Mtandao wa Vikundi vya Wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) katika viwanja vya Mwl. Julius Kambarage Nyerere vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwa ni siku ya nne tangu kufunguliwa kwa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki.

Waziri huyo amesema kwa sasa asali inayouzwa ni 5% tu hivyo Serikali kupitia Wizara hiyo imepanga kuongeza uzalishaji kwa kutoa elimu kwa wafugaji wa nyuki ili waweze kuongeza kiwango cha uzalishaji na kufikia zaidi ya asilimia 50% ya asali inayouzwa nje ya nchi.


“...tunauza asali nje ya nchi 5% mpango wetu wa Wizara ni kuuza tani 148,000 kwa mwaka huu, maana yake ni kwamba tuzalishe tani 148,000 tuongeze uzalishaji kutoka 5% ikibidi tufike hadi 50%...” amesema Waziri Mchengerwa.


Aidha, Mhe. Mchengerwa ameitaka benki ya Azania ambayo inatoa mikopo yenye riba nafuu ya 1% kwa wanawake kutanua wigo wa utoaji wa huduma katika maeneo ambayo hayana matawi ya benki hiyo ili kila mwanamke apate fursa ya mkopo huo.


Akitoa shukrani kwa Waziri huyo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameahidi kuandaa mazingira mazuri ya kuhifadhia wanyama ambao wamekuwa sehem ya kivutio kikubwa cha maonesho hayo.


Sambamba na hilo, Mhe. Adam Malima amesema wataweka utaratibu ili maonesho hayo yasiishie kipindi cha Nanenane pekee utaratibu huo utawezesha maeneo hayo kuendelea kuwa kuvutio.


Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amesema Kanda ya Mashariki inatafsiri kwa vitendo maelekezo na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya uwekezaji katika sekta ya kilimo. 


Kwa upande wake muwakilishi wa Meneja Benki ya Azania Mkoani Morogoro Bw. Josephat Mruma amesema benki hiyo kwa sasa inatoa mikopo ya 1% kwa wanawake ili waweze kujikita katika uzalishaji na kujikwamua kichumi.


Waziri Mchengerwa ametembelea mabanda mbalimbali yaliyopo katika viwanja hivyo na kujionea teknolojia mbalimbali ikiwa leo ni siku ya nne tangu kufunguliwa kwa maonesho hayo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.