• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali kuwachukulia Hatua za kinidhamu Maafisa Ardhi

Posted on: July 13th, 2021

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula amemuagiza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoani Morogoro Frank Mizikunte kuwachukulia hatua za kinidhamu maafisa Ardhi watatu ambao walihamishiwa kikazi Wilayani kilosa ambapo hadi sasa hawajawasili Wilayani humo.

Naibu Waziri Angelina ametoa agizo hilo Julai 12, mwaka huu wakati akifanya mkutano na wananchi wa Tarafa ya Magole kata ya Dumira Mkoani Morogoro ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya siku mbili kwa ajili ya kusikiliza na kutatua migogoro ya Ardhi inayowakabili wananchi wa Wilaya hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula kabla ya kuanza kikao cha kusikiliza  na kutatua kero za  wananchi Wilayani Kilosa.

Naibu Waziri huyo amebainisha kuwa maafisa Ardhi hao ambao wanatakiwa kuchukuliwa nidhamu ni Kasese Ntolela kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, William Njiha kutoka Dodoma Jiji na Hassani Rashidi kutoka Chalinze hawakuwahi kufika Wilayani humo miaka Miwili hadi sasa.

“Hawa watumishi wachukuliwe hatua za kinidhamu, hatuwezi kuendelea kuwa watu ambao tunawahesabu wapo Wilaya ya Kilosa halafu kilosa hawapo huku migogoro ni mingi isiyoisha kumbe kuna watumishi ambao hawajaripoti’’ amesema Mabula.

  1. Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja akiwasalimia wananchi wa Kilosa.

Katika hatua nyingine Dkt. Mabula amesema ni kinyume cha sheria za nchi yetu mwananchi yoyote kumiliki hekali zaidi ya Hamsini bila kuidhinishwa na mkutano mkuu wa kijiji husika ambao ndiyo wenye mamlaka ya kujiridhisha juu ya uhalali wa kukupa eneo la Ardhi zaidi ya hamsini.

Aidha, amezitaka Halmashauri za Mkoa huo kutenga fedha kila mwaka kwaajili ya kupima mipaka ya vijiji ambavyo havijasajiriwa na kuhakikisha kuwa vinapatiwa vyeti vya upimaji huo ili kuondoa changamoto za mipaka ambazo zimekuwa zinajitokeza.

Kwa sababu hiyo, Dkt. Mabula amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja Kuunda kamati itakayohusika na kupima mipaka ya vijiji ambavyo havijasajiriwa na kuisimamia kamati hiyo huku akishirikiana na Wahe. Madiwani wa Halmashauri za Wilaya husika.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema Mkoa huo utaunda timu ya wataalam ili kubainisha mipaka kati ya kijiji na kijiji na kuandaa alama za kudumu hivyo kuepusha baadhi ya viongozi wasio waadilifu kuuza Ardhi nje ya mipaka ya kijiji chao.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Madiwani na watendaji kuwasilisha kwa Kamishina wa Ardhi kumbukumbu zinazobainisha wawekazaji katika kila kijiji ambao wanamiliki Ardhi hizo kinyume na utaratibu hawayaendelezi maeneo wanayomiliki ili waweze kuzifanyia kazi kumbukumbu hizo mapema iwezekanavyo.

Naye Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Morogoro Frank Mizikunte amesema wataanza zoezi la urasimishaji wa Ardhi ili kuepukana na migogoro ya Ardhi ya mara kwa mara inayojitokeza Mkoani Morogoro.

Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria katika Mkutano huo akiwemo Dotto Yohana na Meriyan Mkunda wamesema mabaraza ya kata ya Ardhi ndiyo visababishi vya migogoro hiyo na kuiomba Serikali kuwapatia kitabu cha sheria za Ardhi wenyeviti wa vijiji ili  kuondoa adha ya kuuziwa eneo moja mara mbili.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.