• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali Mkoani Morogoro yawasilisha rasmi taarifa ya Waziri Mkuu Kwa Wananchi wa Chanzuru

Posted on: December 5th, 2020

Serikali Mkoani Morogoro imewasilisha rasmi kwa wananchi wa Chanzuru Wilayani Kilosa mkoani humo maagizo ya Serikali yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kuhusu kumpatia Bw .Miyanga Laizer shamba la Chanzuru lenye ukubwa wa ekari 1,598 kama mmiliki halali wa shamba hilo ikiwa ni utekelezaji wa Kiongozi huyo wa maagizo aliyoyatoa Novemba 30 mwaka huu Ofisini kwake Jijini Dodoma.

Taarifa hiyo imewasilishwa Disemba 4 mwaka huu na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emannuel Kalobelo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Loata Ole Sanare ambaye hakuwepo katika tukio hilo kwasababu ya majukumu mengine ya kikazi.

Akiwasilisha maagizo hayo Mhandsisi kalobelo amesema pamoja na kuwa shamba hilo kwa muda mrefu limekuwa lina mgogoro huku watu mbalimbali wakiuziana shamba hilo na baadae wananchi nao kuwa na matumizi na shamba hilo, na baada ya uchunguzi wa kina Serikali imeamua kumpa Bw. Laizer kwa sababu ya kuwa mmiliki halali na kuonesha dhamira ya kutaka kuliendeleza kwa kulima zao la Mkonge.

Pamoja na sababu hiyo, bado taarifa hiyo iliyotolewa na Mhe. Waziri Mkuu imeeleza kuwa wananchi ambao tayari wako ndani ya shamba hilo kamwe hawataondolewa bali wataendelea kubaki katika makazi yao na kufanya shughuli nyingine walizokuwa wakizifanya awali na Bw.Laizer atapewa fidia ya maeneo hayo kwa kupewa ardhi nyingine nje ya shamba hilo ili kufidia maeneo ambayo tayari kuna makazi ya watu na mashamba ya wanachanzuru.

“sentensi ya pili. Ardhi ndani ya shamba iliyotumiwa na wananchi itambuliwe na wasiondolewe ili kuepusha kusababisha mgogoro mwingine” ilieleza taarifa hiyo

Aidha, taarifa hiyo iliyosomwa kwa umakini mkubwa na Mhandisi Kaloelo kwa lengo la kutaka kufikisha ujumbe wa Serikali, ilieleza kuwa wananchi waliopata maeneo ya kilimo pamoja na Bw. Laizer mwenyewe wanatakiwa kutumia Ardhi hiyo kwa kulima zao la Mkonge.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi aliwaeleza wananchi kuwa Serikali imefikia hatua hiyo ya maamuzi baada ya kufanya uchunguzi wa kina wa shamba hilo ikiwa ni pamoja na kuwa na vikao mbalimbali ambavyo vyote vilikusudia kutatua mgogoro wa shamba hilo la Chanzuru.

Serikali ya awamu ya tano imefikia hatua hiyo kwa sababu ya sera yake ya kuwajali wananchi hususan wanyonge huku mwenyekiti wa kijiji cha Chanzuru Hassan Nengula kwa niaba ya wananchi ameyapokea maagizo hayo ya serikali huku akibainisha kuwa wanayapokea maagizo hayo hasa kama yatafanyiwa kazi kama yalivyosomwa.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.