• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI MKOANI MOROGORO YAJA NA MRADI WA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Posted on: April 30th, 2024

SERIKALI MKOANI MOROGORO YAJA NA MRADI WA UTUNZAJI WA MAZINGIRA


Serikali ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na Shirika la HELVETAS imefanya uzinduzi wa mradi wa Uwezeshaji jamii katika usimamizi endelevu wa misitu (USEMINI) ambapo itasaidia kutunza mazingira kwa kurudisha uoto wa asili na kusaidia kupunguza hewa ukaa.


Uzinduzi huo umefanywa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Aprili 30, 2024 katika hoteli ya Morogoro na na kuhusisha viongozi mbalimbali wa kiserikali na sekta binafsi lengo na kushirikiana katika kutunza mazingira na hivyo kupunguza madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi.

Mhe. Malima amesema kupitia mradi huo utasaidia katika kutunza mazingira na kuondoa hewa ukaa pamoja na kutoa elimu kwa jamii kuhusu upandaji wa miti ya karafuu, kakao, michikichi, kahawa na parachichi  ambayo pamoja na kuwa miti hiyo ni rafiki kwa mazingira, watu na maji bado itawasaidia wananchi kuongeza kipato chao.

“… kwa hiyo kampeni yetu ya Mkoa wa Morogoro ni kupanda miche milioni moja moja ya mazao hayo mbadala kwa ajili ya kurudisha uoto wa miti kwa maeneo ambayo yameharibika kwa kukata miti holela kwa ajili ya mkaa na kilimo….” Amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuna umuhimu mkubwa wa wananchi kupatiwa elimu juu ya matumizi ya nishati mbadala hasa matumizi ya mkaa na kuachana na matumizi ya kuni ambayo yanasababisha wananchi kukata miti kwa ajili ya kupata nishati hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la HELVETAS Daniel Kalimbiya amesema  kwa Mkoa wa Morogoro mradi wa USEMINI unatekelezwa katika Halmashauri 4 ambazo ni Mvomero, Ulanga, Malinyi pamoja na Halmahsauri ya Morogoro DC ambapo utazifikia kaya zaidi ya 2000 zenye wanufaika 10000 kata 20 na vijiji 70 katika Halmashauri hizo.

Hata ivyo Kalimbiya amesema Mradi huo utawajengea uwezo wananchi namna ya kusimamia misitu, namna ya kupanga matumizi bora ya ardhi, namna ya kutumia nishati mbadala, pia mradi huo imekusudia kupanda miche milioni moja ya matunda mbalimbali ili kusaidia kurudisha hali ya kawaida yale maeneo ambayo yameathirika na uharibifu wa mazaingira.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.