• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUSOGEZA HUDUMA ZA KIJAMII KWA WANANCHI

Posted on: September 29th, 2024

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa  na Dkt. Samia Suluhu Hassan imesema imejipanga kuendelea kuwasogezea karibu huduma za kijamii ikiwemo sekta ya Afya wananchi walio maeneo ya pembezoni ili kurahisisha kutofuata huduma hizo kwa umbali mrefu hivyo kuchochea maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.


Kauli hiyo imebainishwa Septemba 29, 2024 na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joseph Masunga wakati wa ziara yake pamoja na wajumbe wa kamati ya siasa ya Halmashauri kuu ya Mkoa huo kwa lengo la kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Mkoa huo, na leo ni siku ya tatu wakiwa Wilayani Ulanga.

Mhandisi Masunga amesema, ilani ya CCM inaitaka serikali kuhakikisha inasogeza huduma za kijamii zikiwemo huduma za Afya, Elimu, Maji, miundombinu ya Barabara na umeme na sekta nyingine kwani amesema huduma hizo ndio msingi mkubwa wa maendeleo ya wananchi.  

"… serikali inatakiwa kuhakikisha kwamba inapeleka huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi na moja ya huduma ya msingi sana ni huduma ya afya…" amesema Mhandisi Joseph Masunga 

Akiwa katika mradi wa Daraja la Chigandugandu lililopo Wilayani Ulanga, Mhandisi Joseph amewataka wananchi kulinda miundombinu ya umma likiwemo Daraja hilo huku akiwashauri kupanda miti ama mazao kama michikichi, mianzi na Migomba pembezoni mwa mto ili kulinda Daraja hilo ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu Tsh. Mil. 107.


Mwenyekiti huyo ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi kujiandikisha kkwenye daftari la kudumu la kupiga kura ili kujihakikishia kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliopangwa kufanyika Novemba 27, 2024 kwani, amesema, hiyo ni haki ya kila mtanzania kupiga kura, kuchaguliwa kuwa kiongozi au kuchagua viongozi bora watakaowaletea maendeleo.

Kwa upande wake, Mjumbe wa kamati ya siasa ya Mkoa huo Bw. Deogratius Mzelu amewapongeza wananchi wa Wilaya ya Ulanga kwa kushirikiana na serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo baada ya wananchi hao kuchangia zaidi ya Tsh. Mil. 12 kwenye ujenzi wa shule ya Sekondari ya Lukande.

Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Lukande Bw. Godfey Senjele amesema ujenzi wa shule hiyo umesaidia kupunguza adha ya wanafunzi wa shule ya Sekondari hiyo iliyopo kata ya Mwaya ambapo walikuwa wanatembea umbali wa 21km kwenda kupata elimu katika sekondari hiyo.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.