• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

serikali yafuta mashamba pori Kilosa Mkoani Morogoro

Posted on: June 8th, 2021

Serikali yafuta mashamba pori 11 Kilosa.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefuta mashamba pori 11 Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro yenye jumla ya Ekari 24,119 na kuyarejesha kwa wananchi ili kuyatumia katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo kilimo na ufugaji.

Taarifa ya kufutwa mashamba hayo imetolewa Juni 7, mwaka huu na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (MB) wakati wa ziara yake Wilayani humo iliyolenga kurejesha mashamba pori hayo kwa wananchi yaliyobatilishwa na Serikali baada ya kuona hayaendelezwi.

Waziri William Lukuvi (MB) akiongea na wananchi wa Kilosa wakati wa Mkutano wa hadhara Juni 7 mwaka huu

“Mwezi wa Nne mwaka huu imempendeza Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kuyafuta mashamba 11 yenye ekari 24,119, na amenituma nije nitoe maelekezo kwamba baada ya kuyafuta mashamba hayo wizara yangu itaunda timu ya wataalamu kuja kufanya tathimini ya  mashamba hayo’’ amesema Mhe. Lukuvi.

‘’.. mashamba yaliyofutwa sehemu watapewe wananchi ambao hawajawahi kumiliki Ardhi na sehemu nyingine watapewa wawekezaji ambao ni waaminifu na hayatagawiwa ovyo.. amesisitiza Mhe. Lukuvi

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa Profesa Paramagamba Kabudi akieleza jambo wakati wa Mkutano huo

Aidha, Waziri Lukuvi amesema mashamba mengine 49 yenye ukubwa wa hekari 45,788.5. yamehuishwa, huku akiwataka wananchi kutovamia mashamba yaliyofutwa kwani watapatiwa kwa utaratibu utakaowekwa mara baada ya kazi ya upimaji kukamilika itakayofanywa na timu ya wataalamu itakayoundwa na akawataka wenyeviti wa vijiji na  chama wahakikishe wanatoa ushirikiano wa kutosha katika kusimamia ugawaji wa mashamba hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema licha ya  Mkoa huo kuwa na migogoro ya Ardhi, ameweka mipango mkakati ya kuhakikisha Migogoro hiyo inaisha ama kupungua na kuufanya Mkoa huo kusifika katika shughuli za maendeleo badala ya kuwa na migogoro ya ardhi muda wote. “watu waamini kwamba Kilosa, Morogoro ni sehemu salama na watu wanaweza kufanya shughuli zao za kimaendeleo” amesema Mhe. Shigela.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Reuben Shigella akitoa nasaha kwa wananchi wa Wilaya ya Kilosa kabla hajamkaribisha mgeni wake Waziri Mhe. William Lukuvi - Juni 7, 2021 

Naye, Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa Profesa Paramagamba Kabudi amesema maamuzi yaliyochukuliwa na Mhe. Rais ya kufutwa kwa mashamba hayo yataweza kupata wawekezaji wenye tija ndani ya Wilaya ya Kilosa na kusaidia Wilaya hiyo kukua zaidi kiuchumi.

Profesa Kabudi


Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilosa Yohana Kasitila na Kamishna Msaidizi wa Ardhi kanda ya Mashariki Frank Minzikuntwe.


DC Kilosa Adam Mgoyi akiteta jambo na RC wake Martine Shigella

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.