• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YAKANUSHA UHABA WA SUKARI NCHINI

Posted on: August 6th, 2023

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imekanusha juu ya uwepo wa uhaba wa sukari hapa nchini na kutoa bei elekezi kwa wauzaji wa bidhaa hiyo ambapo sukari itauzwa kwa Tsh. 2800 hadi 3200 kwa kila kilo moja, hivyo imewataka wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika kwa wale wanaokiuka agizo hilo.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Jokate Mwegelo (kushoto) wakimsikiliza mtaalam kutoka kampuni ya utengenezaji na usambazaji wa mashine na zana za kilimo.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipotembelea banda la Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ikiwa ni muendelezo wa maonesho na Sherehe za Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Julius Kambarage Nyerere vilivyopo katika Manispaa ya Morogoro.

Dkt. Kijaji amesema hakuna upungufu wa sukari hapa nchini kutokana na ongezeko la uzalishaji wa bidhaa hiyo, hivyo amewaelekeza wafanyabiashara wote hapa nchini kuuza sukari kwa bei elekezi ya Tsh. 2,800 hadi 3,200 kwa kilo na kwamba yule atakayekiuka agizo hilo la serikali atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa wawakilishi wa kikundi cha wajasiliamali wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni baada ya kutembelea banda hilo.

“...niwaambie watanzania wawe na amani hatuna upungufu wa sukari na bei ya sukari ni ile ile 2,800 mpaka 3,200, hakuna popote ambapo utaenda utauziwa sukari Tsh. 4,000 ukiuziwa 4,000 toa taarifa sisi tushughulike na huyo anayekuuzia sukari 4,000...” amesema Dkt. Ashatu Kijaji.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akimsikiliza Meneja wa idara ya uelimishaji kutoka Bodi ya sukari.

Aidha, Waziri Kijaji ametoa wito kwa viwanda vyote vinavyozalisha sukari hapa nchini kuongeza uzalishaji na uwekezaji kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya sukari ndani na nje ya nchi.

Aidha, Waziri huyo amesema Serikali inaagiza zaidi ya asilimia 60 ya mafuta ya kupikia kutoka nje ya nchi, hivyo amewataka wakulima hususan wanaozalisha malighafi ya viwanda vya mafuta ya kupikia kuongeza uzalishaji huo kutokana na uwepo wa viwanda vya mafuta 771 kwa kufanya hivyo Serikali itapunguza uagizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi.

Sambamba na hilo, Dkt. Ashatu Kijaji amesema kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Serikali itawafikia wajasiliamali ambao wamekidhi vigezo vya kupata nembo ya utambulisho (tbs) itawapatia bila malipo yoyote lengo ni kuwasaidia kupata masoko zaidi ndani na nje ya nchi.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akisalimiana na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji.

Leo ni siku ya sita tangu kufunguliwa kwa maonesho hayo Agosti 1, 2023 na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda huku  kaulimbiu yake ikiwa ni “Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula”.

MWISHO.










Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.