• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yalia na sekta binafsi kukuza uchumi wa Nchi.

Posted on: August 12th, 2023

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dkt Ashatu Kijaji (Mb.) amesema serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ina mpango madhubuti wa kisera, kisheria na kiutaratibu kushirikiana na Taasisi binafsi ili kutatua changamoto wanazopata na kufufua viwanda.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima wakati wa kikao na wafanyabiashara.


Dkt. Kijaji ameyasema hayo Agosti 11, 2023 wakati akifanya kikao na wafanyabiashara katika ukumbi wa mikutano wa Morena hotel uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa lengo la kusikiliza changamoto zao za kibiashara na kuzitafutia ufumbuzi.



"... Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipoingia madarakani alidhihirisha hadharani kwamba Uchumi wa Taifa letu utajengwa na sekta binafsi... kati ya watanzania Milioni 61.7, walioajiriwa na serikali ni milioni 1 tu na milioni 60.7 waliobaki ni kutoka sekta binafsi..." Amesema Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji.



Kwa sababu hiyo amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka na inaendelea kuweka mazingira mazuri ya kushirikiana na Sekta hiyo kwa kuondoa changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na utitiri wa kodi zisizo na maana.



Katika hatua nyingine Waziri Kijaji amebainisha kuwa dhamira ya Serikali ni kurudisha iliyokuwa Mikoa ya viwanda kuendelea kuwa mikoa ya viwanda kama hapo awali ukiwemo mkoa wa Morogoro ili kuweza kutoa ajira kwa vijana wengi na watanzania wasio na ajira Serikalini na kubainisha kuwa sekta binafsi zina nafasi kubwa katika kukuza biashara na uchumi wa Taifa.



Dkt. Kijaji pia ameishauri Mamlaka ya mapato Tanzania -TRA kutowabebesha mizigo isiyo ya lazima wafanyabiashara kwa kulimbikiza kodi bali ameitaka TRA ishirikiane na wafanyabiashara hao na kuwapa elimu kuhusu ulipaji  wa kodi badala ya kufungia biashara zao lengo ni kuitaka Serikali kukusanya kodi kwa wingi na wafanya biashara kulipa kodi hizo bila shuruti baada kupata elimu ya ulipaji huo wa kodi.



Akisisitiza kuhusu sekta binafsi kuiwekea mazingira mazuri Dkt. Kijaji amesema Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imerekebisha sheria Na.13 zilizokuwa na changamoto kwa wafanyabiashara lengo ni kuweka mazingira mazuri kwa wafanyabiashara hao na kukabidhi uchumi katika sekta hiyo ili uchumi uwe imara ndani na nje ya Nchi.



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akimkaribisha waziri huyo, amemshukuru Waziri kwa kutambua mchango wa wafanyabiashara wa Mkoa huo kwani wanafanya kazi kubwa hususan kuendesha viwanda mbalimbali kama vya sukari, tumbaku, viwanda vya nguo,viwanda vya kuchakata mchele na mazao ya aina ya mikunde n.k. huku akiwahakikishia Ofisi yake kuwapa ushirikiano wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuweka ofisi maalum itakayoshughulikia mashauri yao kwa haraka watakapofika ofisini kwake.


Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa wakati akitambulisha wajumbe wa kikao hicho.

Naye, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Morogoro Fadhili Chilombe, amewahakikishia wafanyabiashara kuwa changamoto ya umeme wanayoipata sasa ni ya kipindi kifupi tu kwani amesema ifikapo mwakani mwezi Juni Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan itakuwa imetatua changamoto hiyo kwa kuwa na umeme wa megawati 700.

Aidha, Mhandisi Chilombe ametoa jibu kuhusu suala la ulipaji kodi ya pango kwa kila mita katika jengo moja, amesema wafanyabiashara wanaopitia changamoto hizo wapeleke ofisini kwake changamoto hiyo ili kuchagua mita moja itakayolipia Kodi.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bi. Beatrice Njau.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.