• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YASHAURIWA KUTOA FEDHA KUTEKELEZA MIRADI YA UTAFITI

Posted on: March 16th, 2023

Kamati ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoshughulikia Elimu, Utamaduni na Michezo imeishauri Serikali kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya utafiti iliyopo hapa nchini.

Ushauri huo umetolewa Machi 15 mwaka huu na Mhe. Kitila Mkumbo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge inayohughulikia Elimu, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya kamati hiyo walipotembelea Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kilichopo Mkoani Morogoro.

“… nitoe wito wetu kama bunge, kuendelea kuiomba serikali kutoa fedha za utafiti ili chuo hiki kiendelee kufanya utafiti na ugunduzi mkubwa na kujiimarisha Zaidi…” amesema Mhe. Kitila Mkumbo.

Aidha, Mhe. Mkumbo amesema wamefurahishwa jinsi chuo hicho kilivyojipanga kutoa wanafunzi mahili na wenye uwezo wa kujitegemea pale watakapohitimu masomo yao.

Wakiwa chuoni hapo, kamati imekagua vitengo vya mafunzo kama kituo cha utafiti na mafunzo ya uchumi wa bluu, hospitali ya Taifa ya rufaa ya Wanyama na jengo mtambuka la mafunzo kuona namna mafunzo kwa vitendo yanavyofanyika na utafiti wa  miradi hiyo inavyofanya kazi na kuongeza pato kwa chuo na Taifa kwa ujumla.  

katika hatua  nyingine Mhe. Mkumbo ametoa wito kwa wanafunzi wa shule hapa nchini kujikita katika masomo ya sayansi na kwenda Kusoma vyuo  vilivyojipanga vema katika kutoa wahitimu mahili kama Chuo Kikuu cha SUA.

Kwa upande wake, Mhe. Omari Juma Kipanga ambaye ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema serikali ina mpango mkakati wa kutekeleza mradi wa HEET (Higher Education for Economic Transfomation) utakaogharimu Zaidi ya Tsh. Bilioni 972, fedha hizo zitapelekwa katika vyuo vyote nchini kushughulikia Sayansi, Teknolojia na Ubunifu.

Waziri Kipanga ametumia fursa hiyo kupongeza jitihada za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. DK. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Tsh. Bilioni 11 kwa ajili ya ujenzi wa jengo linalochukua wanafunzi zaidi ya 300 katika chuo cha SUA.

Nae, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Raphael T. Chibunda amesema kupitia mradi wa HEET chuo kimenufaika kupewa Tsh. Bilioni 73.6 kwa ajili ya kupanua na kuboresha mradi huo wa miaka 5 ulioanza mwaka 2022.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.