• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yataka "SANAA na MICHEZO" kuwa masomo maalum

Posted on: August 17th, 2023

Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imesema iko  mbioni kubadilisha mitaala ya Elimu na kuhakikisha SANAA na MICHEZO yanakuwa masomo maalum lengo ni kukuza vipaji vilivyopo katika sekta hizo, hivyo kutoa ajira nyingi kwa vijana kupitia sekta hizo.

Hayo yamebainishwa Agosti 16 mwaka huu na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Pindi Chana alipotembelea kituo cha kukuza vipaji vya mpira wa miguu (Morogoro kids) kilichopo uwanja wa Mashujaa Mkoani Morogoro  ikiwa ni ziara yake ya kikazi Mkoani humo.

Mhe. Balozi Pindi Chana amesema serikali imedhamiria kubadilisha mitaala ya elimu kwa kutaka masomo ya Sanaa na Michezo kuwa masomo maalum ambapo vijana watafanya michezo hiyo na kujuza vipaji vyao sambamba na kufanya kazi hiyo kwa stadi na weledi mkubwa zaidi.

Mhe. Balozi Pindi Chana akipokea jezi kutoka vijana wa kituo cha Moro kids.

"... ndugu zangu, Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo tumedhamiria kuhakikisha suala la michezo nchini linapewa kipaumbele, hivi sasa tuko katika hatua ya kubadilisha mitaala ya elimu, tunataka masomo ya sanaa na michezo yawe masomo maalum ili tuendelee kukuza vipaji tulivyonavyo..." Amesema Mhe. Balozi Pindi Chana

Aidha, Mhe. Pindi Chana ameagiza kamati za  Wilaya na Kamati ya Mkoa wa Morogoro kukutana ili kujadili changamoto zinazoikabili michezo katika eneo husika ili kutafuta namna ya kutatua changamoto hizo.

Sambamba na hilo, Mhe. Balozi Pindi Chana amempongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya katika sekta ya michezo kwani amesema ameonesha njia na kuwa mfano mzuri na kuifanya Tanzania kuanza kunga'ara kimichezo.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Pindi Chana akiwa pamoja na Viongozi wa Mkoa na Wilaya wametembelea uwanja wa Jamhuri Mkoani humo ili kukagua maendeleo ya maboresho yanayoendelea.

Aidha, Waziri huyo amezipongeza sekta binafsi hususan Taasisi za benki zinavyozidi kumuunga mkono Rais katika suala zima la michezo kwa kuanzia michezo mbalimbali.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameipongeza timu ya Young Africans sports club (Yanga) mabingwa wa kihistoria kwa kujitokeza na kukifadhili kituo hicho cha Moro Kids cha kukuza vipaji hususan mchezo wa mpira wa miguu kwani amesema hatua hiyo itaondoa changamoto ya vifaa kama mipira, jezi n.k na fedha za kuendeshea kituo hicho ambazo zilikuwa zinakikwamisha kituo hicho kufikia malengo yake kikamilifu.

Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mstahiki Meya wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Pascal Kihanga kutafuta eneo zuri na kukitoa kwa kituo hicho cha Moro kids kwa ajili ya kujenga kiwanja cha michezo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiteta jambo na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga.

Naye, Mkurugenzi wa kituo cha Moro kids Prof. Madundo Mtambo ameishukuru Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kutembelea kituo hicho na kuomba eneo ili kuwa na viwanja vya michezo vitakavyo weza kukidhi vijana wengi, kwani kwa sasa wanaopata nafasi ya kupata mafunzo sambamba na  mazoezi ni vijana wachache.

Kituo hicho cha kukuza vipaji vya michezo cha Moro Kids kilianzishwa 1999  na kusajiliwa mwaka 2004 na Baraza la michezo Tanzania.

Hadi sasa kituo kimepata mafanikio makubwa kwa kukuza vipaji vya wachezaji wanaozitumikia timu zao kama Dickson Job, Abtwalib Msheli Kibwana Shomari, Dickson Kibabage, na Zawadi Mauya wakiwa timu ya Yanga na Shomari kapombe na Mzamiru Yasin kutoka timu ya Simba, hivyo ni kituo hicho kinakuza vipaji kwa ajili ya manufaa ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Mwisho.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.