• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yatatua mgogoro wa wananchi wa Morogoro, 367 kulipwa kifuta jasho

Posted on: September 23rd, 2023

Serikali yatatua Mgogoro wa wananchi wa Mindu, 357 kulipwa kifuta jasho.

 

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imemaliza mgogoro wa muda mrefu wa Kata ya Mindu, kwa kuwalipa kifuta jasho wananchi 357 na wengi wao kuruhusiwa kubaki katika makazi yao lakini kwa kufuata miongozo ya Serikali ili kulinda Bwawa la Mindu ambalo ni tegemeo la wananchi wa Manispaa ya Morogoro katika upatikanaji wa maji.


Kauli hiyo ya Serikali imetolewa Septemba 22, 2023 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry William Silaa (Mb) alipofanya ziara ya siku moja Mkoani Morogoro na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Mindu ili kutatua mgogoro uliokuwa unaleta mvutano baina ya wananchi na Serikali.

Akitoa kauli hiyo, Waziri Jerry Silaa amesema kwa mujibu wa nyaraka za Wataalam zilizopo, tayari watu waliokuwa wanaishi eneo la Bwawa la Mindu miaka ya 1979 walishalipwa fidia na walielekezwa Kwenda eneo la Mafuru Wilayani Mvomero, hivyo kwa sasa hakuna mwananchi anayestahili kulipwa fidia tena isipokuwa wananchi 357 kupewa kifuta jacho.

Akibainisha zaidi Mhe. Waziri amesema wananchi 357 wanaostahili kupewa kifuta jasho na kuondoka eneo la Mindu ni wale wanaoishi ndani ya Mita 500 kutoka Bwawani na walio nje ya mita hizo wataendelea na makazi yao lakini kwa kufuata miongozo yote itakayotolewa na Serikali kwa lengo la kulilinda Bwawa hilo kwa maslahi mapana ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mhe. Waziri amesema, Pamoja na kuwapatia kifuta jasho wananchi 357 wanaotakiwa kuhama, bado Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa busara zake amewataka wananchi hao kuwpatia kiwanja kimoja kila mmoja katika eneo la CCT ili wakaendeleze Makazi yao eneo hilo.

"Dkt. Samia amenielekeza kwa utaratibu ule ule wa hekima, busara na huruma yake kwa wananchi 357 nikuelekeze Kamishna Msaidizi wa Ardhi kuhakikisha wanapata viwanja na huo uwe mkono wa heri kwao ili tulinde hili bwawa Kwa faida yetu..." amesema Mhe. Jerry Silaa.

Hata hivyo, Waziri huyo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa na huruma, busara na hekima kwa watu wake, na kuonya vikali wananchi watakaokiuka taratibu hizo hekima haitatumika tena bali sheria zitafuata mkindo wake.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akimkaribisha Mgeni wake Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema yupo tayari kupokea maelekezo yote kutoka serikalini na kuyasimamia kama miongozo inavyoelekeza.

Kwa upande wake, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Morogoro Bw. Frank Minzikuntwe amewasihi wananchi waliobaki ambao wako nje ya mita hizo 500 kuheshimu na kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutoendeleza maeneo hayo huku akisikitishwa na baadhi yao kuendelea na ujenzi wa makazi rasmi kabla ya kurasimishwa maeneo hayo.

Sambamba na hayo Bw. Frank amewataka wananchi hao kuwa wavumilivu kutoendeleza makazi yao hadi hapo watakapomaliza zoezi la urasimishaji Ardhi linalotarajiwa kuanza hivi karibuni ili kuepusha migogoro ya Ardhi ya mara kwa mara inayojitokeza Mkoani Morogoro.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.