• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YATENGA 1.2 UJENZI WA GATI MTO MNYERA

Posted on: June 15th, 2022

Serikali yatenga 1.2 Bil. kwa ajili ya ujenzi wa gati

Serikali imetenga jumla ya  Shilingi   bilioni 1.2  kwa ajili ya kujenga gati mbili kwenye mto mnyera kwa ajili ya kuweka kivuko kitakachosaidia  kuunganisha   wilaya ya  Malinyi na Kilombero  Mkoani Morogoro na hivyo kuongeza ukuaji wa uchumi kwa wananchi wa Wilaya hizo mbili.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela {mwenye kofia katikati}akiwa eneo la ujenzi wa gati la Mto mnyera upande wa Wilaya ya Malinyi

Akizungumzia faida ya ujenzi wa Magati hayo mawili na kuweka kivuko, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro MARTINE SHIGELA amesema licha ya kusaidia kuunganisha wilaya hizo mbili lakini ujenzi huo pia kutasaidia kurahisisha mawasiliano ya mikoa miwili ya Morogoro na Njombe.

mto Mnyera

Akibainisha zaidi kuhusu ujenzi huo Martine Shigela amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imetenga jumla ya shilingi Bil. 3.2Bil kwa ajili ya ujenzi wa gati mbili kwa maana ya pande mbili za mto Mnyera ujenzi utakaogharimu shilingi 1.2 Bil.


Lakini pia amesema Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini - TARURA wamepewa shilingi 1.5Bil. kwa ajili ya ujenzi wa barabara zitakazounganisha magati hayo mawili kila upande wa mto mnyera yaani gati la kila upande na kisha wataongezewa shilingi 500 Milioni watakazopewa kwa awamu mbili kila awamu shilingi 250Milioni na kufanya jumla ya shilingi 3.2 Bil.

Shigela amebainisha kuwa lengo la Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hasssan kujenga kivuko hicho ni kurahisisha usafirishaji wa mazao ya wananchi wa wilaya hizo mbili na mikoa jirani lakini pia Mkoa wa Morogoro unakwenda kufikia kirahisi mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma kupitia kivuko cha mto Mnyera. 

“Upande wa TANROADS tayari wameshatenga fedha 1.2 Bil.watajenga gati huku  na watajenga gati upande wa pili ili kuunganisha na kuleta kivuko sit tu kwa ajili ya kusafirisha binadamu bali pia kusafirisha mazao ya kibiashara” amesema Martine Shigela.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Mhe. Pius Mwelase (mwenye koti jekundu) akiwa pamoja na baadhi ya viongozi walioambatana na RC katika msafara wake

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka TARURA wa pande zote mbili za Mlimba na Malinyi kuhakikisha kutumia vizuri bajeti ya fedha zilizotengwa ili kuhakikisha barabara hizo zinafunguka, huku akiwataka wananchi kujipanga kuzalisha kisasa na kutumia hiyo fursa inavyotakiwa na kuendelea kulinda na kutunza mazingira  ya mto Mnyera kwa kuwa mto huo ni moja ya vyanzo vikuu vya bwawa la kufua Umeme la Mwlimu Nyerere.

Wa kwanza kushoto  ni DAS Malinyi na wa pili ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Fortunatus Muslim

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi PIUS MWELASE amesema kivuko hicho kitasaidia wananchi kwenda mikoa ya jirani kwa shghuli za kijamii ikiwemo kupata huduma za matibabu katika Hospitali ya Ikonda iliyoko Mkoa wa Njombe lakini pia kivuko hicho kitaongeza mapato ya Halmashauri yao.

 

Naye Ditram Mhenga Diwani wa Kata ya Utengule iliyoko upande wa pili katika Halmashauri ya Mlimba Wilaya ya Kilombero amesema kukamilika kwa kivuko hicho kutaongeza uchumi  wa halmashauri hizo mbili kupanda kwani eneo hilo baada ya kufunguka litavuta wawekezaji kuwekeza katika sekta hiyo ya kilimo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.