• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yatenga Tsh. Bil. 28.1 Sekta ya Mifugo.

Posted on: January 4th, 2025


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt. Ashatu Kijaji (MB)  amesema Serikali ya awamu ya sita imetenga fedha shilingi Bil 28.1 kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025 kwa ajili ya sekta ya mifugo pekee kwa ajili ya kutekeleza mapinduzi ya sekta hiyo ikiwemo kufanya kampeni ya chanjo ya mifugo ili kuhakikisha mifugo hapa nchini inakuwa na ubora unaohitajika kimataifa.

Waziri Kijaji amesema hayo Januari 4, 2025 Wilayani Mvomero katika Kijiji cha Kambala ambacho ni maalum kwa ajili ya wafugaji ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani Morogoro.

Akifafanua zaidi, Waziri Dkt. Ashatu  Kijaji amesema, fedha hizo zimelenga kutoa chanjo za homa ya mapafu ya ng'ombe,  ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo na ugonjwa wa kuku wa kideli huku fedha nyingine kutumika kununua pikipiki 700 na vishikwambi 4500 kwa ajili ya maafisa ugani wa mifugo ili kurahisisha utendaji kazi wao hivyo kutimiza maono ya Rais Samia.

"...Kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 60 tangu tupate uhuru, Mama katupa Tsh. Bil. 28.1  kwa ajili ya wafugaji tu..." amesema Dkt. Ashatu Kijaji.

Aidha, Waziri amemuagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na uvuvi anayeshughulikia Mifugo kufanya utafiti wa haraka ili kujenga kisima au bwawa katika kijiji cha Kambala kabla ya bajeti ya mwaka 2025/2026 ili wafugaji hao kuacha kufuata maji umbali mrefu na kusababisha migogoro baina yao na wakulima.

Katika hatua nyingine, Waziri Ashatu Kijaji amewataka wafugaji kwenda na kasi ya mapinduzi ya sekta hiyo na kutekeleza kwa vitendo utaalamu wanaopewa na maafisa ugani kwani amesema Mhe. Dkt. Samia Suluhun Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana dhamira ya dhati ya kuhakikisha mapinduzi ya sekta hiyo yanafanikiwa.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa wa Morogoro una agenda ya mapinduzi ya mifugo kwa kupata mbegu za mifugo hasa ng'ombe ambao watafugwa kisasa na kuondokana na Mkoa kuwa na mifugo mingi isiyo na tija, badala yake kuwa na mifugo michache lakini yenye ubora na inayokidhi masoko ya nje.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amesema migogoro mingi baina ya wakulima na wafugaji Mkoani humo inasababishwa na ukosefu wa maji, kwani amesema wafugaji wanapotafuta maji kwa ajili ya mifugo yao mara nyingi mifugo yao hupata nafasi ya kula mazao ya wakulima hivyo amemuomba Waziri kuchimba kisima kwenye kijiji cha Kambala ili wananchi wake kupata maji ya uhakika kwa ajili ya mifugo yao.

Naye Askofu Jacob Mameo wa Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Morogoro amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa na mchango chanya katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya mifugo kwani amesema migogoro iliyokuwa ikizikumba Wilaya za Kilosa na Mvomero miaka ya nyuma imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na juhudi za serikali hii ya awamu ya sita.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.