• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yatoa Mil. 193 kusaidia kaya maskini.

Posted on: July 29th, 2021

Serikali kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya  Maskini - TASAF  imetoa kiasi cha shilingi Mil. 193 kwa ajili ya ujenzi  wa  wodi moja  ya wazazi katika zahanati ya  kata ya  Mkambarani iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro lengo likiwa ni kuwapunguzia adha ya kutembea mwendo mrefu kutafuta huduma ya Afya.

Akizungumza  na wananchi wa kata hiyo Julai 27 mwaka huu, Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Deogratius Ndejembi  amesema  kutolewa kwa fedha hizo kunatokana na maombi ya wananchi waliyoyatoa kupitia viongozi mbalimbali wa chama na Serikali juu ya adha wanayopata katika kupata huduma ya Afya.

Aidha, Ndejembi ametoa onyo kali juu ya matumizi sahihi ya pesa iliyotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa wodi hiyo na kumtaka Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando kusimamia vizuri ujenzi huo ili fedha hizo zisitumike kinyume na maagizo ya Serikali.

"Kusitokee mchwa wa kutafuna fedha hizi, hatutamfumbia macho maana wapo baadhi ya watu wakishaona fedha Kama hivi wanawaza kuzitafuna tu, DC simamia ujenzi huu na wasitumike wakandarasi hapa itumike force akaunti" amesema Ndejembi.

Sambamba na hayo, Ndejembi amewataka wenyeviti wa vijiji na mitaa kutenda haki katika uandikishaji wa kaya maskini na kuacha hila wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo ili kila mwananchi anayestahili kuwa katika mpango wa TASAF apate haki yake.

Kwa upande wake Mratibu wa TASAF Wilaya ya Morogoro Bi. Austaki Moshi, amesema mpango huo wa kunusuru kaya maskini umeleta manufaa katika Kijiji cha Mkambarani ikiwemo watoto kuhudhuria kliniki na kusaidi wanafunzi kuhudhuria kwa wingi Shuleni  kutokana na huduma nzuri zinazotolewa.

Pia Bi. Austaki amesema jumla ya wanafunzi 110 wanasoma na kupatiwa mahitaji ya elimu kwa kutimiza masharti ya mpango huo katika shule ya msingi Mkambarani.

Awali,  akiwasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mkambarani, Mbunge wa jimbo la Morogoro kusini Hamisi Tale Tale, maarufu kama Babu Tale amesema amekuwa akipata malalamiko mengi kutoka kwa wazee wasiojiweza juu kutoandikishwa katika mpango wa TASAF hali inayopelekea  wazee hao kuishi katika maisha ya dhiki.

Naye Mkuu wa wilaya ya Morogoro Albert Msando amekiri kupokea maagizo ya Naibu Waziri huyo na kumuhakikishia kutekeleza maagizo yote aliyoagiza ili kutimiza adhma ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri y Muungano wa Tanzania ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Mpango wa  kunusuru kaya maskini - TASAF awamu  ya tatu ni mpango wa Kitaifa ambao unatekelezwa Tanzania bara na Zanzibar. Mpango huu ulizinduliwa rasmi na Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 22 Agosti 2012, Jijini Dodoma.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.