• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YATOA TSH. 250 MIL. KWA AJILI YA KUJENGA, KUKARABATI MADARAJA MAWILI WILAYANI ULANGA

Posted on: June 12th, 2024

Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza ujenzi wa Daraja moja na jingine kukarabatiwa katika Kijiji cha Chigandugandu na Mbuga Wilayani  Ulanga Mkoani Morogoro baada ya madaraja ya awali kuathiriwa na Mvua za Elinino za mwaka huu na kusababisha adha kwa wananchi wa maeneo hayo.


Hayo yamebainika Juni 12, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa ziara yake akiambatana na Wajumbe wa KUU ya Mkoa huo ya kukagua miundombinu mbalimbali na utekelezaji wa Maelekezo ya Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa (MB) aliyoyatoa wakati wa ziara yake takribani mwezi mmoja uliopita.

Mhe Adam Malima amesema, Waziri Mchengerwa alifanya ziara Mkoani Morogoro kujionea hali ya Mafuriko yalivyoukumba Mkoa wa Morogoro na baada ya kufika eneo la Daraja la Mbuga alitoa ahadi kwa niaba ya Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kujenga madaraja hayo mawili ya Kamba ili kuwaondolea adha wananchi hivyo amefika kufuatilia utekelezaji wa fedha hizo.

“sisi leo tumekuja kuangalia maendeleo ya kazi ya zile milioni 250 zilizotoka kwa ajili ya kurekebisha haya madaraja mawili” amesema Adam Kighoma Mhe. Malima.

Amesema, uharibifu wa madaraja hayo mawili umechangiwa kwa vikubwa na shughuli za kibinadamu hasa kilimo kinachofanyika pembezoni mwa mto unaojengwa madaraja hayo mawili na akatumia fursa hiyo kuwataka wananchi kutofanya shughuli za kilimo ndani ya mita sitini kila upande wa mto au kulima mazao rafiki yanayozuia mmomonyoko wa ardhi.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala ya Barabara za Mjini na Vijijini – TARURA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emanuel Ndyamkama amesema, madaraja hayo mawili yanajengwa baada ya kupokea fedha kutoka Serikalini na yatajengwa kwa kipimo cha kuwezesha kupita waenda kwa miguu, pikipiki za magurudumu mawili na zile za magurudumu matatu – Toyo pekee ili kurahisisha wananchi kuvusha mazao yao lakini pia kuyafanya yadumu kwa muda mrefu.

Aidha, Mhandisi Ndyamkama amesema Baada ya mafuriko ya Mvua za Elinino za mwaka huu, wamefanya tathmini na kugundua kuwa Mkoa wa Morogoro una uhitaji wa madaraja 64 ya aina hiyo ya madaraja yanayojengwa eneo hilo ambayo thamani yake ni Tsh. Mil. 200 kwa kila Daraja moja la Kamba.

Naye Diwani wa Kata ya Ilonga Habiba Abdallah Katundu kwa niaba ya wananchi wake, amemshukuru Rais kwa  kupeleka fedha za kujenga Daraja moja jipya na kukarabati jingine ambayo yote ni ya Kamba, hii ni kutokana na athari za mafuriko kubomoa madaraja hayo, hivyo kukamilisha madaraja hayo kutarahisisha usafirishaji wa bidhaa ambayo ndio kichocheo cha Uchumi wa eneo hilo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.