• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI YATOA TSH MIL. 800 KUREJESHA MIUNDOIMBINU MALINYI

Posted on: May 21st, 2024

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 800 kwa ajili ya kujenga Daraja la mto Furua ili kuondoa changamoto ya usafiri na usafirishaji inayowakabili wananchi wa Wilaya hiyo.


Hayo yameelezwa leo Mei 21, 2024 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa (MB) wakati akiendelea na ziara yake Mkoani humo.

Ni siku ya pili ya ziara ya Waziri Mchengerwa akiwa Mkoani Morogoro ambapo leo Mei 21, 2024 yupo Wilayani Malinyi na kukagua miundombinu ya barabara za Mji wa Malinyi na kujiridhisha kuwa miundombinu hiyo imeharibiwa vibaya na mafuriko yaliyotokea hivi karibuni na kwa niaba ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Waziri ametoa fedha hizo kwa ajili ya kujenga Daraja la Mto Furua ikiwa ni suluhisho la muda.

Hata hivyo, amuagiza Meneja wa Wakala ya Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Ndyamukama kutafuta mkandarasi wa kujenga Daraja la Mto huo na kukamilisha ndani ya kipindi cha wiki mbili ili kuwawezesha wananchi wa Malinyi kusafirisha nafaka na bidhaa mbalimbali ambazo ni muhimu kwao na kwa Uchumi wa Taifa.


“…nimeshawaelekeza watendaji wa Wizara yangu Mkurugenzi wa Ujenzi TAMISEMI anayewasimamia TARURA na Meneja wa TARURA wameniambia wanahitaji Mil. 800, nimewapa wiki mbili nataka Barabara hii ipitike…’’Amesema Waziri Mchengerwa.

Sambamba na hilo, Mhe. Mohamed amewataka viongozi wa ngazi zote kushirikiana  na kuwa wabunifu ili kuwatumikia wananchi kikamilifu huku akiwaagiza Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara kuitisha vikao vya dharura na wataalamu wote ndani ya Mikoa yao pamoja na wadau wa Maendeleo ili kujadili na kurejesha mawasiliano ya Barabara zilizoharibiwa na mafuriko.

Katika hatua nyingine, Waziri Mchengerwa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za dharura kwa lengo la kukarabati miundombinu mbalimbali ikiwemo Barabara kutokana na athari za mafuriko yaliyotokea maeneo mbalimbali hapa nchini.


Akimkaribisha Waziri huyo wa TAMISEMI, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Mhe. Mchengerwa kwa maamuzi yake ya haraka kwa kutoa fedha Tsh. Mil.800 kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la mto Furua na kuonya kuwa asiwepo kiongozi ama mtu yeyote kujaribu kufuja fedha za Mradi huo ili Daraja litakalojengwa lilingane na fedha zilizotolewa (Value for Money).

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Malinyi Mhe. Said Tila kwa niaba ya wananchi wa Malinyi, pamoja na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumtuma mwakilishi wake kutoa pole za mafuriko na kuona athari zake, amebainisha changamoto wanazozipitia ikiwa ni pamoja na bei za bidhaa kupanda.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.