• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yawataka wananchi kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Posted on: August 2nd, 2024

Serikali imewataka wananchi kuwa na mpango endelevu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kushirikiana na wataalam na watafiti wa mazingira ili kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao ya kilimo, ufugaji na uvuvi wenye tija.


Ushauri huo umetolewa Agosti 2, mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwenye uzinduzi wa maonesho ya nanenane kanda ya mashariki yanayofanyika katika viwanja vya nanenane vilivyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani Morogoro.


Akifafanua zaidi Mhe. Batilda amesema wananchi wanapaswa kutumia nishati safi kama umeme, gesi na mkaa mweupe ili kuepukana na mabadiliko hayo katika kutunza vyanzo vya maji, misitu na ardhi ili kutunza rutuba yake kwa uzalishaji wa mazao bora.


“… tunapaswa kuzingatia matumizi ya nishati safi kukabiliana na mabadilio ya tabia nchi…” amesema Mhe. Batilda Burian


Aidha, Balozi Batilda amesema maonesho hayo yameendelea kuwavutia wadau mbalimbali kila mwaka kwani mwaka 2023 kulikuwa na washiriki 75,000 na mwaka 2024 waliojiandikisha ni zaidi ya 80,000 na kubainisha kuwa maonesho hayo yataendelea kutoa elimu kwa wananchi katika kufanya shughuli za kilimo, Uvuvi na ufugaji kwa kutumia teknolojia zaidi.  


Sambamba na hilo, Mhe. Burian amesema sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi inatoa nafasi za ajira kwani 65% wanajishughulisha na kazi hizo, ambapo 28% huchangia pato la taifa, 24% ya mauzo ya bidhaa za mazao hayo nje ya nchi.


Hata hivyo Mhe. Batilda amesema serikali itaendelea kuimarisha ushirika, vikundi na majukwaa ya wadau wa kilimo, mifugo na uvuvi ili kuunganisha nguvu kuwa na sauti ya pamoja katika kuimarisha matumizi sahihi ya rasilimali.


Mhe. Batilda amewasisitiza wakulima, wafugaji na wavuvi kushiriki kikamilifu na kujitokeza katika kugombea nafasi mbalimbali za uchaguzi na kuwachagua viongozi bora ambao watahimiza shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji na kuwasaidia katika masuala ya biashara na kuwa na tija katika taifa.


Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Kampuni ya Viridium ya Tanzania amesema kampuni hiyo imechukua hatua za mapema kuanza kutoa elimu kuhusu matumizi ya nishati mbadala ikiwemo mkaa mweupe ambao hutengenezwa kwa majani maalum aina ya briquettes kuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Maonesho hayo hufanyika kila mwaka Agosti 8 kwa lengo la kutoa elimu kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ambapo kitaifa maonesho hayo yanafanyika Mkoani Dodoma.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.