• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yawataka wananchi waishio mabondeni kuhama

Posted on: September 25th, 2023

Serikali imewatahadharisha wananchi      waishio maeneo ya mabondeni kuhama ili kuepuka athari za Mvua za Elnino zinazotarajiwa kunyesha kuanzaia mwezi Oktoba mwaka huu kama ilivyoelezwa kwenye taarifa ya Mamlaka ya Hali ya hewa Nchini (TMA).


Hayo yameelezwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe, Ummy Hamis Ndeliananga Septemba 25, 2023 wakati akifungua kikao kazi cha kuimarisha Kamati za Usimamizi wa Maafa za Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kilichokuwa na lengo la kuzuia na kupunguza madhara ya Elnino.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Ummy ameitaka Mikoa na Halmashauri zote hapa nchini kuwa na mipango ya utekelezaji katika maeneo yao katika kukabiliana na mvua za Elnino lakini kwa kuzingatia Mipango ya Taifa iliyotolewa kwao.

“Mikoa na halmashauri iandae mipango ya utekelezaji katika maeneo yao kwa kuzingatia Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Nino”. Amesema Naibu Waziri.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Sebastian Waryuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo kusafisha mitaro ya kupitisha maji katika maeneo yao hususan katika kipindi hiki cha mvua ili kuepuka mafuriko yatayosabiabisha magonjwa ya mlipuko.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya kwa niaba ya MKuu wa Mkoa amewataka wananchi Mkoani humo wanaoishi maeneo ya mabondeni kuhama makazi yao Kwenda maeneo ya miinuko kwani amesema kinga ni bora kuliko tiba.

Akiwasilisha wasilisho lake katika kikao hicho, Meneja wa TMA kanda ya mashariki Bi. Hidaya Senga amewashauri wananchi kupata taarifa za hali ya hewa kupitia njia mbalimbali lakini zilizothibitishwa na TMA kwa kuwa taasisi hiyo ndiyo pekee hapa nchini  yenye mamlaka ya kutoa taarifa hiyo.


Sambamba na hilo Bi Hidaya amewaomba waandishi wa Habari kutoa taarifa za hali ya hewa zile zilizohuishwa na Mamlaka ya Hali ya hewa Nchini kwa kutumia lugha rahisi, yenye kueleweka na bila kuleta mtafaruku kwa jamii.


Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro Goodluck Zelote amesema tayari jeshi hilo limeuchukua hatua za mapema kukabiliana na janga la Elnino ikiwemo kuainisha maeneo Korofi yanayopata mafuriko mara kwa mara, kuandaa vifaa vya uokozi, kuandaa rasilimali watu Pamoja na kutoa elimu kwa wanachi namna ya kujikinga na mafuriko.

Kwa mujibu wa utabiri wa Mamlaka ya hali ya hewa Nchini mikoa 14 itakayoathirika na mvua hizo zitakazoanza kunyesha Oktober mwaka huu hadi Mwezi Januari 2024 ni Pamoja na Mkoa wa Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, kusini mwa mkoa wa Simiyu, kaskazini mwa mkoa wa Kigoma, Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikiwemo visiwa vya Mafia) na kaskazini mwa mkoa wa Morogoro.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.