• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serikali yazishirikisha sekta binafsi zikiwemo taasisi za kidini katika shughuli za Maendeleo

Posted on: September 28th, 2023

Serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imejizatiti kukuza uchumi wa nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi zikiwemo taasisi za kidini kama Kanisa katoliki Jimbo la Morogoro kujikita katika shughuli za kiuchumi hususan Kilimo, Utalii, Elimu, Mawasiliano na huduma ya afya kwa manufaa ya wananchi.


Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Muhagama katika ibada ya Shukrani ya kutimiza miaka 25 ya upadri wa Mhashamu Askofu Lazarus Vitalis Msimbe wa Jimbo katoliki la Morogoro iliyofanyika kwenye viwanja vya misionari ya mtakatifu Peter iliyopo kata ya Kilakala katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

"...Jimbo hili limeendelea kushiriki katika maendeleo mengi katika jamii ambapo mpo kwenye sekta ya Afya, Elimu, Mawasiliano na sekta nyingine nyingi..." amesema Mhe. Jenista Muhagama

 

Mhe. Muhagama amesema taasisi za kidini zinaombwa kuwekeza katika huduma mbalimbali ikiwemo Elimu, Kilimo, afya na nyingine nyingi kwani Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amejizatiti kushirikiana na taasisi hizo kupunguza vifo visivyokuwa na lazima ili kuwa na nguvu kazi ya uhakika hapa nchini.

Aidha, Mhe. Muhagama amewataka wazazi/walezi kuiga mfano wa wazazi wa Askofu Lazarus Vitalis Msimbe kuwalea watoto wao kwa kuzingatia utamaduni, Mila na desturi za nchi kwani utandawazi una mifumo inayoweza kuharibu watoto sambamba na vijana ambao ndio tegemeo la Taifa.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo amewatahadharisha watanzania kuhusu mvua za El-nino baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  kutoa utabiri wa mvua hizo, hivyo amesema ni jukumu la watanzania wote kushirikiana ili kukabiliana na maafa pale yatakapojitokeza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema inatakiwa taasisi za kidini ikiwemo kanisa katoliki la Morogoro kuendelea kuwekeza katika shughuli za kiuchumi hususan katika Utalii na Kilimo ambapo amebainisha mazao ya kibiashara yakiwemo  karafuu, hiliki, Kakao yanayolimwa Mkoani humo na kuahidi Ofisi yake ya Mkoa kutoa ushirikiano kwa  taasisi hiyo kama itahitaji kuwekeza katika kilimo hicho.

Sambamba na hilo, Mhe. Malima amesema  Kanisa hilo liendelee kukemea ukatili wa watoto, mauaji ya vikongwe na albino sambamba na kukemea ndoa za jinsia moja kwani hukwamisha shughuli za maendeleo ambapo ndio chachu ya kukuza uchumi wa Taifa.

Nae, Mhashamu Askofu Lazarus Vitalis Msimbe wa Jimbo katoliki la Morogoro pamoja na  kutoa shukrani  zake kwa wote waliohidhuria ibada hiyo ameitaka jamii kumtegemea Mungu na kutenda matendo mema kwa jirani na jamii kwa ujumla.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.