• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Serkali Mkoani Morogoro yajivunia PJT MMMAM, yaahidi kuweka mikakati kuiendeleza.

Posted on: August 31st, 2023

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Bw.  Anza-Ameni Ndosa amesema wanajivunia mafanikio ya program Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT – MMMAM) ambayo imewajengea watoto Mkoani humo mazingira mazuri ya kujifunzia, upatikanaji wa lishe bora na kuwawezesha wazazi na walezi kutoa malezi bora.

Anza-Ameni Ndosa amesema hayo Agosti 29, 2023 wakati akifungua kikao cha mapitio ya utekelezaji wa Programu hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Amesema Serikali ilianzisha programu hiyo mwaka 2021 ambayo inatekelezwa katika Mikoa 26, Mkoa wa Morogoro ukiwa miongoni mwa mikoa hiyo kwa kushirikiana na shirika la Childhood Development Organization (CDO) kutekeleza programu hiyo katika Halmashauri zote 9 za Mkoa huo na kubainisha kuwa hiyo imehamasisha watoto kupata chakula wakiwa shuleni na kusaidia idadi ya watoto wanaojiunga na elimu ya awali kuongezeka.

“...tunajivunia mafanikio tuliyoyapata hadi sasa na tutaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha kuwa kila mtoto katika Mkoa wa Morogoro anapata fursa sawa na kuanza maisha yao wakiwa na msingi imara...tutaendelea kufanya kazi na wadau ili kuendeleza programu hii...” amesema Bw. Ndosa.

Akielezea lengo la Programu MMMAM ambayo ilizinduliwa Mkoani humo Mei 23, 2023, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Morogoro Bi. Delfina Pacho amesema, lengo programu hiyo ni kuondoa changamoto za watoto walio chini ya miaka 8 na kikao hicho kinajadili utekelezaji wa programu ngazi ya Mkoa na Halmashauri ili kubaini mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa programu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Childhood Development Organization (CDO) Bi. Felistas Kalomo amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii katika Halmshauri za Mkoa wa Morogoro kutekeleza agizo la Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Dorothhy Gwajima (Mb) lililotaka kufungia vituo vyote vya kulea watoto mchana (Day Care) ambavyo havijasajiliwa na havikidhi vigezo vya kupokea watoto.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.