• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SH. BILIONI 100 ZATENGWA KUJENGA VYUO 64 VYA UFUNDI NCHINI.

Posted on: March 13th, 2023

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetenga Tsh. bilioni 100 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa vyuo 64 vya fundi stadi ngazi ya Wilaya na chuo kimoja cha ufundi cha Mkoa wa Songwe.

Mhe. Omari Kipanga Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia akizungumza na washiriki mbalimbali wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa watekelezaji wa mafunzo ya mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi.

Hayo yamebainishwa Machi 10, 2023 mwaka huu na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Juma Kipanga (MB) wakati akifungua mafunzo kwa watekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF.

“…mwaka 2022/2023 serikali imetenga bilioni 100 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vyuo stadi 64 katika ngazi ya wilaya na Chuo kimoja katika Mkoa wa Songwe, yaani katika Mikoa 26 ya Tanzania bara, Mikoa 25 tayari tumeshajenga isipokuwa Mkoa mmoja ambao ni Mkoa wa Songwe ambapo kwa bajeti hii ya 2022/2023 tunakwenda kujenga chuo hicho…” amesema Mhe. Omari Juma Kipanga.

Washiriki wa mafunzo kwa watekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi wakimsikiliza Mhe. Omari kipanga Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo.

Aidha, Mhe. Kipanga amesema lengo kuu la serikali kujenga vyuo hivyo ni kutaka vijana wa kitanzania kuwa na uwezo wa kujiajiri, kuajiriwa, kuondoa changamoto ya ajira na kukuza uchumi wa nchi.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kipanga amewataka watekelezaji hao kukamilisha ujenzi wa majengo  9 kwa Kila Wilaya ifikapo mwezi Septemba Mwaka huu kwa Ubora unaotakiwa na kwa kulinganisha na kiwango cha fedha kilichotolewa ( Value for money).

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa Bi. Germana Mung'aho amesema vyuo hivyo vitawasaidia vijana wa elimu mbalimbali ili kukuza maendeleo ya Morogoro na taifa kwa ujumla, hata hivyo amesema Mkoa wa Morogoro unatarajia kuwa na vyuo viwili vya ufundi stadi ambavyo bado vipo kwenye hat ha za ujenzi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, na Teknolojia Mhe. Omari Juma Kipanga (Mb) (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa watekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.