• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Shigela aagiza TANROADS Morogoro kukagua madaraja

Posted on: October 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoani humo kuhakikisha anajiridhisha na uimara wa madaraja na makaravati yote ya Mkoa huo kuwa yako salama kabla ya msimu wa mvua haujawadia.

Martine Shigela ametoa agizo hilo Oktoba 5, mwaka huu wakati wa ziara yake ya siku moja Wilayani Kilosa iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kutatua kero za wananchi katika  Tarafa ya Magole.

Mradi wa kwanza alioutembelea Mkuu huyo wa Mkoa wakati wa ziara hiyo ni pamoja na ujenzi wa daraja la Kiegea lililoanza kujengwa rasmi Novemba 5, mwaka jana kazi ambayo ilitarajiwa kukamilika ndani ya miezi sita na kushindwa kukamilika  kutokana na sababu mbalimbali.

Akiwa katika mradi huo pamoja na kupongeza hatua iliyofikiwa ya asilimia 90 ya  ujenzi wa daraja hilo, alimtaka mkandarasi kukamilisha kazi hiyo kwa muda ulioongezwa huku akitumia fursa hiyo kumuagiza Meneja wa TANROADS kupitia madaraja na makaravati yote ya Mkoa huo kuyafanyia matengenezo yanayohitaji kukarabatiwa kabla ya msimu wa mvua haujaaza.

“kwa hiyo nimekuja kufanya ukaguzi, tunaelekea masika na nimuelekeza Meneja wa TANROADS matatizo tuliyoyapata mwaka jana tusiyapate mwaka huu, kwa hiyo tujiridhishe madaraja yote na makaravati yote toka mpakani mwa Pwani mpaka mpakani mwa Dodoma tuyapitie makaravati yote na kutoka mpakani mwa Pwani mpaka mpakani mwa Iringa…..aliagiza Martine Shigela.

Akifafanua kuhusu umuhimu wa barabara na watumiaji wake, Shigela amesema barabara zinaposimama kwa sababu ya ubovu kimsingi zinasimamisha Uchumi wa eneo husika na wa taifa nzima kwani watu mbalimbali hawatafanya kazi wakiwemo madereva, watu wa Bandarini, wauza mafuta, nyumba za wageni na wafanyabiashara wengine watasimama kufanya kazi na kusababisha madhara makubwa kwa nchi kiuchumi.

Katika hatua nyingine, Martine Shigela amempongeza Mkandarasi anayejenga daraja la Kiegea Eng. Aloyce Stephen ambaye ni mzawa, kwa kutekeleza kazi hiyo kwa uaminifu huku akiwataka wakandarasi wengine wazawa kuiga mfano wa Mkandarasi huyo kufanya kazi kwa uzalendo ili kuondoa dhana iliyojengeka kuwa wakandarasi wazawa hawawezi kufanya kazi zao kikamilifu mara wanapopewa tenda hizo.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa ujenzi wa daraja hilo la Kiegea ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu  shilingi za kitanzania Bil. 6.9 Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro Eng. Baraka Mwambage alimueleza Mkuu wa Mkoa sababu zilizokwamisha ujenzi huo kuchelewa zikiwemo  za kiufundi na wingi wa mvua, kwani mwezi mmoja baada ya kuanza kazi hiyo  zilianza kunyesha.

Hata hivyo Eng. Mwambage alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa ujenzi wa daraja hilo utakamilika ndani ya wiki mbili zijazo yaani kabla ya mwezi Novemba mwaka huu magari yote yataanza kupita juu ya daraja hilo la Kiegea.

Kwa upande wake Mkandarasi wa mradi huo Eng. Aloyce Stephen alieleza changamoto iliyomfanya kuchelewa kukamilisha kazi ya ujenzi huo kuwa ni kutokana na baadhi ya vifaa vya ujenzi kuchelewa kuletwa eneo la ujenzi kutoka Dar es Salaam huku akimhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa kazi hiyo itakamilika kabla au ifikapo  Oktoba 30 mwaka huu.

Akiwa katika kata ya Berega Mkuu wa Mkoa alikagua ubovu wa Daraja la Beraga ambalo mara kadhaa limeleta adha kwa wananchi hususan akinamama wanaokwenda kupata matibabu katika hospitali ya Berega.

Diwani wa kata ya Berega Elikana Masonda kwa niaba ya wananchi alieleza adha wanayopata wananchi wake kipindi cha masika hususan wananwake wanapokwenda kupata huduma za Afya katika hospitali ya Berega hulazimika kusubiri maji yaliyojaa kupungua ndipo waendelee na safari jambo ambalo ni usumbufu kwa wagonjwa na akina mama.

Hata hivyo Diwani huyo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa Tsh. Bilioni 7.9 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo ambao linatarajiwa kuanza muda wowote kuanzia sasa.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa ametembelea Kata tatu za Mtumbatu na Dumila ambako alifanya mikutano ya hadhara na kutatua kero za wananchi pamoja na kata ya Berega ambako alitembelea madaraja hayo mawili ya Kiegea na daraja la Berega.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.