• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SHIGELA AONYA MADALALI WA MIWA WANAODHULUMU WAKULIMA.

Posted on: May 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ametoa karipio kwa madalali wa zao la miwa wasio waaminifu hivyo kutumia nafasi zao na kuwadhulumu wakulima wa zao la Miwa wa Wilaya za Kilombero na Kilosa Mkoani Morogoro.





Shigela ametoa karipio hilo Mei 12 Mwaka huu katika ziara yake ya kutatua Kero za wananchi hususan wa Kikundi cha AMCOS cha wakulima wa miwa wa Kijiji cha Sanje Kata ya Sanje Wilayani Kilosa Mkoani humo.



Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa Madalali ya kusaidia wakukima wao wamekuwa chanzo cha wakulima kupoteza haki zao za msingi ikiwemo kutonufaika vema na zao hilo la Muwa, ambapo ametaka kuondoshwa madalali hao ili wananchi waweze kunufaika na zao hilo kwa kujiletea maendeleo yao.



“Wapo Madalali hawana mashamba ya Miwa lakini kila Mwaka ni wauzaji wa Miwa pale. Mwaka huu hakuna hata mtu mmoja atakayeuza Miwa asiyekuwa na shamba, wale mliojipanga kufanya hivyo mkatafute biashara nyingine ya kufanya vinginevyo mtaenda kuozea jela na hili namaanisha.." amesema Shigela.

Katika hatua nyingine Martine Shigela ameoneshwa kukerwa na makato mbalimbali ya tozo zilizo nje ya mkataba wa uvunaji wa Miwa ambazo zimekuwa mzigo mzito kwa wakulima na kusababisha wakulima hao kuendelea kuwa masikini.




Akisoma masharti na vigezo vya kumpata Mkandarasi wa Uvunaji wa Miwa Bwana Jackson Mushumba ambaye ni Afisa Ushirika wa Kanda Bonde la Kilombero amesema, mojawapo ya Masharti hayo ni Mkandarasi kuwa na magari yaliyo bora kiutendaji kwa ajili ya kusafirisha Miwa, AMCOS zilizo na DRD kuanzia 150 zinatakiwa kuajili wakandarasi wawili na mkandarasi awe tayari kukatwa kwenye malipo yake ili kufidia hasara atakazosababisha kwa mkulima ikiwemo kutofikisha Miwa kiwandani kwa wakati au kutupwa kwa Miwa njiani kutokana na kuzidisha uzito wa miwa Kwenye gari.



Naye Bi. Elizabeth Masheyo kwa niaba ya wakulima na wanakijiji wa kijiji Cha Sanje ameshauri Makandarasi kuweka Kambi zao Kijijini hapo na kuajiri wavunaji wa Miwa wanaoishi katika eneo hilo ili kuwezesha shughuli zingine za kiuchumi kujua Kijijini hapo ikiwemo kuinua mzunguko wa pesa kwani kwa sasa mzunguko wa pesa umekuwa mdogo kwa kuwa wakataji miwa wengi hawatoki Kijijini hapo bali wanatoka eneo jirani la Ruaha.




MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.