• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SHIGELA ATOA MAELEKEZO KWA MAAFISA UTUMISHI

Posted on: May 1st, 2022

SHIGELA ATOA MAELEKEZO MAZITO

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewataka viongozi wa Serikali na Taasisi zake Mkoani humo hususan wanaohusika na kupandisha madaraja ya watumishi kufanya hivyo bila kusukumwa na bila kusubiri muda wa mwishoni uliotolewa na Serikali wa kupandisha madaraja hayo kwa watumishi wanaostahili.




Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (wa tatu kulia) akitoa zawadi na cheti kwa mmoja wa Mfanyakazi Bora Marijani Mwaya anayefanya kazi kutoka katika Ofisi yake 


Shigela ametoa agizo hilo Mei Mosi mwaka huu wakati wa maadhimisho ya siku ya Wafanya kazi duniani ambayo huadhimishwa Mei Mosi kila mwaka ambapo Kwa Mkoa wa Morogoro sherehe hizo zimefanyika Mikumi Wilayani Kilosa.

“Ipo tabia ya kusubiri dakika za mwisho ndipo tunaanza kukumbushana muda wa promotion unanataka kuisha, kwa hiyo niombe sana Maafisa Utumishi mfanye hivyo, na kwa kweli naamanisha wala sitanii”. ameagiza Shigela.





Baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama walioshiriki maadhimisho ya Mei Mosi


Meza Kuu wakiwemo Wabunge Mhe. Profesa Paramagamba Kabudi Mbunge wa Jimbo la Kilosa (kulia) na Mhe. Denis Londo wa Jimbo la Mikumi (wa pili kulia). kushoto kabisa Ni Dkt. Rozalia Rwegasira Kaimu Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Morogoro. wengine ni viongozi wa shirikisho la vyama vya Wafanyakazi TUCTA 

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Maafisa Utumishi kutekeleza majukumu  yao ya kupandisha na kushusha vyeo vya watumishi bila kumuonea yeyote wala kuangalia upande mmoja wa kushusha vyeo vya watumishi kuliko kuwapandisha na kuangalia stahili zao.

Mbali na maagizo hayo Mkuu huyo wa Mkoa amekemea kwa baadhi ya Wakuu wa Taasisi, Idara na halmashauri ambao hawajibiki kupeleka zawadi za wafanya kazi bora siku yasherehe ya Mei Mosi ambao wamewachagua badala yake kuahidi kulipwa siku nyingine jambo ambalo ametaka lisirudiwe tena.




Wasanii wa Mashairi wenye ulemavu wa kuona wakiimba shairi lao lililokuwa na maudhui ya Mei Mosi ambalo liliwagusa watu wengi



RC Shigela akiwa katika picha ya pamoja na waimba mashairi



watu waliwatunza waimba mashairi


MKuu wa Mkoa akishirikiana na Kaimu RAS kuhesabu michango ya fedha iliyotolewa kwa ajili ya washairi

Sambamba na hayo Martine Shigela amewataka waajiri wa watumishi wa Umma kuwaruhusu wafanyakazi wao kuwa na vyama vyao mahali pa kazi lakini pia kuwaruhusu kushiriki sherehe za Mei Mosi.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo amewataka wafanyakazi nao kufanya kazi kwa bidii na kutekeleza majukumu waliyopewa kwa weledi na uaminifu masaa yote ya kazi ili kuiletea maendeleo Taasisi husika na Taifa zima kwa ujumla.


Burudani nyingine zilikuwepo. hapo ni umoja wa wasanii wa muziki kutoka Kilosa wakiburudisha na meza kuu kujikuta wako jukwaani

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA kupitia Risara yao iliyosomwa na Katibu wa TALGWU  Mkoa wa Morogoro Bi. Hellen Kobelo mbele ya mgeni rasmi imeeleza changamoto mbalimbali ambazo bado zinawakabili watumishi Serikalini na Sekta binafsi ikiwemo kero ya kutopandishwa vyeo au madaraja kwa wakati pamoja na kucheleweshewa kurekebishiwa mishara kwa wale waliopandishwa na kwamba upandishwaji huo wa madaraja umekuwa si wa weledi.


Aidha, wameiomba serikali kuiagiza Idara ya kazi na Uhamiaji kuendelea kufanya kaguzi za mara kwa mara kwenye sehemu za kazi hasa mashambani na migodini ili kubaini uhalali wa wageni wanaofanya kazi katika maeneo mbalimbali hapa nchini na kuchunguza mikataba na vibali walivyo navyo.


Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kilosa Profesa Paramagamba Kabudi mbali na kuwahakikishia watumishi kuwa yeye pamoja na wabunge wengine watahakikisha wanawapambana kwa ajili ya maslahi yao ya kiutumishi ambayo bado hawajatekelezewa amesema watumie fursa ya filamu ya Royal Tour iliyozinduliwa hivi karibu na Mhe. Samia Suluhu Hassan kutangaza Mbuga ya wanyama ya Mikumi.

Wahe. Wabunge wa Jimbo la Kilosa (kulia) na Jimbo la Mikumi Dennis Londo

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilosa Yohana Kasitila (mwenye trucksuit) akipongezwa na Mkuu wake wa Wilaya hiyo Majid Mwanga kwa kutambuliwa kwake kuwa mmoja wa wafanya kazi Bora

Mwisho, amewahamasisha wawekezaji  wazawa kuwekeza katika mji wa Mikumi na Kilosa kujenga hoteli zenye viwango vya juu kwa ajili ya watalii watakaoanza kumiminika katika Mbuga hiyo baada ya kuhamasishwa na filamu ya Royal Tour.



MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.