• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Shigela atoa mwezi mmoja kwa usajili feki

Posted on: June 16th, 2021

RC shigela awashauri Bodaboda Gairo, atoa mwezi mmoja kwa wenye pikipiki zenye usajiri feki

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ametoa mwezi mmoja kwa waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda Wilayani Gairo kusajili pikipiki zao kihalali kwani imefahamika kuwa baadhi ya waendesha pikipiki hao pikipiki zao zina usajili ulioandikwa kwa mkono ambapo ni kinyume cha sheria.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela

Martine Shigela ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa Hadhara na wananchi wa Mji wa Gairo ikiwa ni mara ya kwanza KWA Mkuu huyo kuongea nao wananchi hao tangu ateuliwe na Mhe. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuuongoza Mkoa wa Morogoro.

Katika hotuba yake Mkuu huyo wa Mkoa amesema, Wilaya ya Gairo ni moja ya Wilaya zenye changamoto ya uhalifu ukiwemo wizi wa pikipiki ambao mara kadhaa umepelekea baadhi yao kupoteza pikipiki zao na hata maisha yao kwa kukodiwa na baadhi ya wahalifu na kisha kuwapora pikipiki na kuuawa.

Mhe, Martine Shigela RC  Morogoro akiteta jambo na Katibu Tawala wa Mkoa huo Mariam Mtunguja (kushoto) 

Kwa sababu hiyo Shigela amewataka Bodaboda wote Wilayani Gairo kwanza, kuwa makini na watu wanaowabeba na kuwataka wawapeleke maeneo tofauti, lakini pili bodaboda hao wanapaswa kutoa ushirikiano kwa Serikali, kwa maana ya polisi na kutoa taarifa zenye uhakika katika kukabiliana na wahalifu hao ili wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Hata hivyo Martine Shigela ametoa mwezi mmoja kwa pikipiki zote ambazo hazijasajiliwa ama zimesajiliwa isivyo halali kusajili pikipiki hizo ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Juni 14 mwaka huu, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wataobainika wana pikipiki zisizo na usajili halali au zimesajiliwa isivyo halali.

“Nipongeze kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya, nipongeze na DC umeshatoa maelekezo mahususi na maelekezo haya ni maelekezo ya Mkoa mzima wa Morogoro, kama kuna pikipiki zimeandikwa kwa mkono na wakati tunahangaika kuwatafuta wezi…..tunawapa ndani ya mwezi mmoja wazisajili kihalali” ameagiza Martine Shigela.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Siriel Mchembe yeye aliwahakikishia wananchi namna Serikali ya awamu ya sita ilivyojidhatiti katika kupunguza kero kwa wananchi na kutoa mfano wa hivi karibuni ambapo Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyopunguza faini za makosa ya bodaboda kutoke shilingi elfu thelathini hadi elfu kumi.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Siriel Mchembe

Kabla ya Mkuu wa Mkoa kupewa fursa ya kuongea, wananchi wa Gairo walitoa kero wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja uwepo wa wizi wa pikipiki hususana katika kata ya Magoleko, pamoja na kamata kamata ya bodaboda inayofanywa na Polisi Wilayani humo jambo ambalo tayari Mhe. Mkuu wa Mkoa amepiga marufuku kuwakamata hovyo vijana hao tena wakiwa wamevaa kiraia.

RC Martine Shigela akivishwa skafu na vijana wa sakauti

 RC na DC Gairo wakionekana wakicheza wakati  wakikaribishwa uwanjani kwa ajili ya Mkutano

Changamoto nyingine ambazo wananchi waliziwasilisha mbele ya Mkuu wa Mkoa ni pamoja na upungufu wa dawa katika kituo cha Afya cha Gairo na kukosekana wa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) katika kituo hicho.

Rachel Nyangasa (kulia) Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo wakati wa mkutano wa hadhara

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.