• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SHIGERA ATAKA UJENZI WA MAJENGO YA UVIKO KUJENGWA USIKU NA MCHANA

Posted on: June 3rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewaagiza Viongozi Mkoani humo kukamilisha ujenzi wa majengo ya UVIKO – 19 kabla au ifikapo Juni 30 mwaka huu kwa kufanya kazi hiyo usiku na mchana na kuongeza wataalamu wakiwemo wakandarasi na mafundi.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akikagua jengo la huduma ya dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Mvomero wakati ziara yake Wilayani humo, kushoto mwa Mkuu wa Mkoa ni Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Halima Okash.



RC Morogoro (mwenye shati la maua) akipokelewa na baadhi ya wahandisi ali[potembelea site ya ujenzi wa wa Jengo la Dharura


Martine Shigela ametoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa ziara yake ya siku moja Wilayani Mvomero alipotembelea ujenzi wa miradi ya maendeleo na kutatua kero za wananchi ambapo alikagua Ujenzi wa Jengo la Dharura katika Hospitali ya Wilaya hiyo, lenye thamani ya shilingi 300 Mil. zilizotolewa na Serikali.



Amesema, Majengo hayo ya kimkakati ambayo fedha zake zinatokana na program ya UVIKO - 19 hazitakiwi kuvuka mwaka huu wa fedha 2021/2022 lakini pia malengo ya fedha hizo zilizokopwa kutoka shirika la fedha Duniani – IMF yaweze kutimia na serikali kuaminiwa hivyo kuweza kupewa mkopo mwingine wa masharti nafuu kwa maendeleo ya wananchi wake.



Kwa sababu hiyo, Mkuu wa MKoa Martine Shigela ametoa maelekezo ya kufanya kazi ya ujenzi wa miradi hiyo usiku na mchana na kuongeza wafanyakazi ili kukamilisha ujenzi wa majengo kwa muda uliopangwa.

“kwa hiyo hakikisheni kama ambavyo nimeeleza hapa, ujenzi ufanyike usiku na mchana…lakini kama kuna mahala ambapo mnaweza kuongeza wataalamu hakikisheni mnaongeza wataalamu hasa wajenzi, wakandarasi na mafundi…” ameelekeza Shigela.



Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan imetoa jumla ya Shilingi 690,000,000.00 kwa ajili ya kuongeza baadhi ya majengo muhim ya Hospitali ya Wilaya ya Mvomero ambayo iko Km.1.5 kutoka Barabara kuu  ya Dodoma – Morogoro likiwemo Jengo la Dharura, nyumba ya watumishi (3 in One), wodi ya wanawake, kichomea taka na njia za kutembelea wagonjwa katika Hospita hiyo.

 

Muonekano wa jengo la dharura katika Hospitali ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.




MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • RAIS MSTAAFU WA AFRIKA KUSINI AWATAKA WAAFRIKA KUENZI MASHUJAA WAO.

    May 23, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.