• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SUMA JKT yatakiwa kuweka mpango mkakati kuendeleza shamba la ekari 12,000.

Posted on: June 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adama Kighoma Malima amemuagiza Meneja wa shamba la SUMA JKT Mngeta Plantation lililoko Wilayani Kilombero Mkoani humo Meja Gaudensi Msaka kuandaa Mpango mkakati utakaoonesha  uendelezaji wa shamba hilo lenye ukubwa wa ekari 12,000 kwa lengo la kukuza sekta ya kilimo hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ( wa pili kushoto) akiwa pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ( wa kwanza kulia), Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Danstan Kyobya na Meja Gaudensi Msaka kwenye shamba la mpunga.

Mhe. Adam Malima ametoa agizo hilo Juni 8 mwaka huu akiwa Wilayani Kilombero wakati wa ziara ya kutembelea Halmashauri zote tisa za Mkoa huo na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kila Halmashauri hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akijaribu moja kati ya mitambo inayotumika katika shughuli za uzalishaji katika shamba hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, kuendeleza shamba hilo, inahitaji uwekezaji mkubwa kwa sababu hiyo amemtaka  Meneja wa shamba hilo na viongozi husika wa shamba la JKT SUMA Mngeta Plantation kuandaa andiko litakaloonesha namna ya kuboresha uendeshaji wa shamba hilo kwa tija.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akijionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanywa na SUMA JKT.

“...nimeongea nao na nimewaambia wakatengeneze andiko la kuendeleza ekari 10,000 kati ya ekari 12,000 za shamba hili...” amesema Mhe. Adam Malima.

Aidha, Mhe. Adam Malima amesema benki za hapa nchini zina uwezo wa kutoa fedha ambazo zinaweza kutumika katika kuendeleza shamba hilo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameonesha kufarijika kuona shamba hilo liaendelezwa na SUMA JKT na namna Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyojithatiti kuwatumikia wananchi wake.

Kwa upande wake Meneja wa shamba la SUMA JKT Mngeta Plantation Meja Gaudensi Msaka amesema kuwa mpango wao kwa sasa ni kuwashirikisha wataalam mbalimbali wa kilimo wa ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao yanayolimwa kwenye shamba hilo kutoka  gunia 15 hadi kufikia gunia 30 au zaidi.

Baadhi ya mitambo inayotumika katika shamba la Mngeta Plantation.

Amesema, kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023 uongozi ulipanga kulima ekari 5,500 ambapo tayari ekari 2,000 za mpunga zimeshalimwa, huku wakiwa katika maandalizi ya kulima ekari 3,500 za mahindi na msimu wa mwaka 2023/2024 wanatarajia kulima ekari 9,000 huku msimu wa 2024/2025 wanatarajia kulima ekari zote 12,000 ambapo ekari 7000 ni za mahindi na ekari 5,000 zitalimwa mpunga.

Awali shamba la SUMA JKT Mngeta Plantation lilikuwa likiendeshwa na KILOMBERO PLANTATION Ltd (KPL) na sasa linaendeshwa na SUMA JKT wakizalisha mazao ya mpunga na mahindi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.