• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

Posted on: March 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa – TAKUKURU Mkoani humo  kufuatilia matumizi mabaya ya fedha za Serikali zaidi ya Shilingi Mil. 500,000,000/=  zilizotumika katika ujenzi wa kituo cha Afya cha  Duthumi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Agizo hilo amelitoa Machi 12, mwaka huu wakati wa ziara yake ya kikazi Wilayani humo ya kukagua miradi ya maendeleo ya sekta ya  Afya na Elimu  ambapo alifika katika kituo hicho cha Afya, kukagua maendeleo ya ujenzi wake na kugundua ubadhirifu wa fedha hizo.

Loata Sanare amesema kuwa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  alitoa Shilingi Mil. 500,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kituo hicho cha Afya ambapo fedha hiyo ilitumika bila kukamilisha majengo yaliyokusudiwa.

Aidha, amesema licha ya fedha iliyotolewa na Mhe. Dkt. John Pomnbe  Magufuli kutokamilisha majengo hayo, Halmashauri iliongezea Shilingi Mil. 72,000,000/= zilizotokana na mapato ili kukamilisha ujenzi wa  majengo hayo ambapo kwa mara nyingine Mkurugenzi akalazimika kuongeza silingi Mil. 25,000,000/=.

 ‘’Kila kituo cha Afya wametoa Milioni 400, na baadhi ya maeneo kwa sababu ya umbali walipewa Milion 500, na hapa kukawa na ubadhilifu mkubwa wa fedha hali iliyopelekea baadhi ya watu kuchukuliwa hatua, na Milion 100 mliyoongezea ingetosha kukamilisha majengo yote muhimu’’ amesema Loata Sanare

Wakati wa ziaya yake katika eneo hilo la Duthumi wananchi walipata fursa ya kutoa changamoto zinazowakabili ambapo kati yake hizo walimuomba Mkuu wa Mkoa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) kwa ajili ya ya kituo cha Afya Duthumi.

Wakielezea mateso wanayopata  Bi. Mwanahawa Mohamed, amesema licha ya kituo hicho kuhudumia Tarafa mbili za Bwakila chini na Mvuha hakuna gari la wagonjwa  hivyo wagonjwa wakizidiwa hulazimika kutafuta gari kutoka Mamlaka ya uhifadhi wa Wanyama Pori Tanzania - TAWA au kutoka tarafa ya Ngerengere ambayo iko mbali na Kituo hicho.

Changamoto nyingine iliyowasilishwa mbele ya Mkuu wa Mkoa na Chesco Raulent ni wauguzi  kuchelewesha kutoa kibali maalumu (Rufaa) kwa wagonjwa waliozidiwa kwenda kupata huduma ngazi ya Hospitali ya Wilaya, hali ambayo hupelekea wagonjwa  kupoteza maisha.

Kwa upande wake Kaimu DMO wa kituo hicho Kasole Maungo, amekiri kuwepo kwa changamoto ya gari ya wagonjwa ambapo amesema TAMISEMI inatarajia kutoa magari ya wagonjwa matano moja kati ya hayo italetwa katika kituo cha Afya Duthumi.

‘’Kuna vituo vitano ambavyo TAMISEMI wamesema yatakuja magari katika vituo vitano na kituo ambacho kitapewa gari mpya ni hiki hapa, kwahiyo kuhusu Ambulance TAMISEMI italeta’’ amesema Maungo .

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.