• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TAASISI ZA KIBENKI ZATAKIWA KUTAFUTA MBINU MPYA ZA KUMSAIDIA MKULIMA

Posted on: January 30th, 2022

Taasisi za kibenki zatakiwa kutafuta mbinu mpya za kuwasaidia wakulima.

Taasisi za kibenki hapa nchini zimetakiwa kutafuta mbinu na utaratibu mzuri utakaosaidia wakulima kupata mikopo yao kwa wakati na kwa masharti nafuu ili kuendeleza kilimo chenye tija na kukuza uchumi wao na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde (Mbunge) Januari 28 mwaka huu wakati wa kikao kazi cha viongozi wa vyama vya ushirika vya wakulima wa Miwa hapa nchini (Agricultural Marketing Cooperative Society - AMCOS) na Taasisi za kibenki kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Sukari cha Taifa kilichopo Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde akiwa kwenye kikao kazi baina ya wakulima wa miwa na taasisi za kibenki, Mkoani Morogoro, Januari 28 mwaka huu 

Agizo hilo limekuja baada ya viongozi wa vyama hivyo kumweleza Naibu Waziri changamoto wanazokutana nazo mara wanapohitaji mikopo kwenye taasisi za kibenki ikiwa ni pamoja na riba kubwa, masharti mengi pamoja na kupata mikopo hiyo wakati msimu wa kilimo umeshapita.

Kwa sababu hiyo, Naibu Waziri Mavunde amezitaka Taasisi hizo za kibenki, kila benki kwa namna yake kutafuta utaratibu unafaa kwao na unaoweza kushawishi wakulima kwenda kukopa lakini mikopo itakayotoka wakati wa kilimo au muda walioomba wakopaji na si vinginevyo.

“ kwenu ninyi mabenki ndio wakati mwafaka sasa, mmeshaona changamoto kubwa inayosemwa ni namna ya kuweza kutoa mikopo kwa wakati ili wakulima wawahi msimu. njooni na utaratibu ambao utamfanya mkulima awe confortable kuja kwako. Lakini mwongozo wetu ni kwamba lazima mikopo yetu iendane na msimu wa mazao ya wakulima ili wasipishane nao” amesisitiza Naibu Waziri Mavunde.

Mhe. Mavunde akipokelewa na baadhi ya viongozi mkoani Morogoro wakati wa ziara yake, kulia ni Mrajisi msaidizi Mkoa wa Morogoro Kenneth Shemdoe

Aidha, pamoja na Serikali kupongezwa kutokana na kuazishamfumo mpya wa uvunaji miwa Kijiografia (ZONE), Naibu Waziri ameiagiza Bodi ya Sukari hapa nchini kwa kushirikiana na Vyama vya Ushirika kuanzisha mfumo huo mpya wa uvunaji miwa kijiografia katika maeneo mengine yenye wakulima wadogo wa miwa lengo likiwa ni kukomesha changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza hapo awali.

Wakiwa katika kikao hicho, baadhi ya Viongozi wamelalamikia suala la Ukomo wa Madeni ambapo Naibu Waziri Mhe. Anthony Mavunde amemwelekeza Mrajisi wa Vyama vya Ushirika hapa nchini kushughulikia suala hilo haraka ili mkulima asinyimwe fursa ya kukopesheka katIka taasisi za kibenki kwa sababu ya changamoto ya ukomo wa madeni.

Baadhi ya Viongozi wa vyama vya ushirika (AMCOS) vya wakulima wa zao la miwa wakiwa kwenye kikao kazi kilichofanyika Chuo cha sukari cha Taifa Mkoani Morogoro

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Denis Londo amemueleza Naibu Waziri changamoto ya wakulima wa miwa kuwa ni pamoja na pembejeo za kilimo kuwa juu hususan Mbolea lakini pia mbolea hizo kutopatikana kwa wakati na kumuomba Waziri kuichukua changamoto hiyo na kwenda kuifanyia kazi.

Mbunge wa jimbo la Mikumi Mhe. Denis Londo 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari hapa nchini Prof. Kenneth Bengesi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, aliwaeleza wajumbe nia ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuendelea na mpango wa kupanua viwanda vya Sukari vya Kilombero, Mtibwa na Kagera ili kuondoa changamoto ya upatikanji wa sukari hapa nchini.

Mkurugenzi wa bodi ya sukari Tanzania Prof. Kenneth Bengesi akiongea wakati wa kikao hicho

Awali, Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Uchumi na uzalishaji Mali Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira amemshukuru Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde kwa kufanya ziara katika mkoa huo na kutoa maaelekezo ya serikali ambapo alikiri kuwa watayatekeleza yote na kwa wakati.

Aidha, Dkt. Rozalia amesema zao la miwa mkoani humo linategemewa zaidi na kufafanua kuwa takribani tani 1,700,000 zinazalishwa kwa mwaka na zao linalofuata ni  mpunga linalozalisha tani 900,000 kwa mwaka na kumjulisha Waziri kuwa mkoa huo  una chakula cha ziada tani 1,300,000.

Dkt. Rozalia Rwegasira akiongea katika kikao hicho

Kwa upande wa wakulima wa miwa akiwemo Habibu Nakanoga ambaye ni Katibu wa Miwa AMCOS Kilombero wameipongeza serikali kwa kuanzisha utaratibu wa uvunaji miwa kwa kuzingatia jiografia (ZONE) na kusema kuwa utaratibu huo umeonekana una tija kubwa kwa wakulima wa miwa wa Kilombero ambapo msimu huu wameonekana kufanya vizuri ukilinganisha na misimu iliyopita.

Mkulima wa miwa Leonard Deogratias kutoka Misenyi Mkoani Kagera ambaye ni mwenyekiti wa AMCOS ya Bubale, pamoja na kuzitaka Taasisi za kibenki kuwafikia na kuwakopesha kama wanavyofanya kwa wakulima wa miwa wa Morogoro pia ameomba uongozi wa Bodi ya Sukari na Serikali kwa jumla kwenda kuwatengenezea utaratibu wa ZONE ili kuondosha changamoto walizo nazo.

Baadhi ya Viongozi wa vyama vya wakulima wa miwa wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde (Katikati ya waliokaa) 

Kwa mujibu wa Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Kenneth Shemdoe ametaja baadhi ya faida za uvunaji miwa kwa kutumia utaratibu wa Kijiografia (Zonning) kuwa ni pamoja na kusaidia kudhibiti magonjwa kwenye mazao ya miwa, kwa kuwa kazi hiyo hufanywa kwa pamoja kama zone badala ya mtu mmoja mmoja.

Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Kenneth Shemdoe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Kilimo (Hayupo pichani) wakati wa kikao cha wadau wa kilimo cha zao la miwa

Faida nyingine alizozitaja za mfumo wa uvunaji miwa kijiografia ni pamoja na urahisi wa kupitisha miundombinu, kupunguza changamoto za mioto, wepesi wa kupata takwimu sahihi za uzalishaji wa zao la miwa pamoja na kukomesha tabia ya utoaji na upokeaji rushwa wakati wa mavuno ya zao hilo.


MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.