• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TANROADS MOROGORO YAONGEZEWA BAJETI

Posted on: October 7th, 2021

TANROADS Morogoro yaongezewa bajeti

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kutoa fedha katika Mkoa wa Morogoro  kwa ajili ya matengenezo ya barabara na miundombinu mingine na kuongezeka kutoka Tsh. Bil. 24.8 mwaka 2020/2021 hadi  kufikia Tsh. Bil. 26.02 mwaka 2021/2022.

Katibu Tawala wa Mkoa wa morogoro Mariam Mtunguja akitoa maneno ya utangulizi kabla ya Mkuu wa Mkoa hajafungua kikao hicho

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela wakati akifungua kikao cha 37 cha Board ya Barabara Mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Ualimu Morogoro leo Oktoba 7, 2021.

RC Morogoro Martine Shigela akifungua kikao cha 37 cha Road Board

Mkuu huyo wa Mkoa ameendelea kuwaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa kwa upande wa Bajeti ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ilikuwa Tsh. Bil. 2.75 na kuongezeka hadi Tsh. Bil. 5.37 mwaka 2021/2022 zikiwemo Tsh. Bil. 2.4 iliyotolewa kwa ajili ya Barabara ya Bigwa – Kiloka Km. 15 kwa kiwango cha lami.

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Paramagamba Kabudi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la kilosa akitoa mchango wake wa mawazo kwenye kikao cha Road Board Mkoani Morogoro


Baadhi ya Wahe. Wabunge wa Mkoa wa Morogoro wakichangia hoja kwenye kikao hicho

Aidha imeelezwa kuwa Bajeti ya matengenezo ya barabara za vijijini na Mijini chini ya Wakala wa Barabara TARURA katika mwaka wa fedha 2020/2021ilikuwa shilingi Bil. 8.07 na mwaka huu 2021/2022 bajeti imeongezeka kufikia Tsh. Bil 8.23.


Baadhi ya Wakuu wa Wilaya wa Mkoa wa Morogoro wakichangia hoja

Kwenye bajeti ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 chini ya TARURA ilitengwa bajeti ya Tsh. Mil. 400 na mwaka 2021/2022 bajeti imeongezeka hadi kufikia Bil. 23.93.

Wakijadili sekta hiyo ya Miundombinu ya Barabara Wajumbe walio wengi wa kikao hicho walionekana kufurahishwa na utendaji kazi wa TANROADS na TARURA Mkoani humo huku wakiwataka watendaji hao kuongeza juhudi kiutendaji badala ya kubweteka na pongezi zilizotolewa kwao na wajumbe wa kikao hicho .

MWISHO 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.