• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

TMDA yakasimisha mamlaka ya ukaguzi wa dawa

Posted on: June 7th, 2022

Mamlaka ya dawa na vifaa tiba Tanzania (TMDA) imekasimisha mamlaka ya ukaguzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa wataalamu wa maabara, Wafamasia na waganga wa mifugo wa Halmashauri kwa lengo la kukagua na kudhibiti changamoto ya bidhaa hizo kutumika pasipo na ubora.


Meneja wa TMDA Kanda ya Kati Bi. Sonia Mkumbwa akizungumza wakati wa mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa dawa vifaa tiba, na vitendanishi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TMDA Kanda ya Kati Bi. Sonia Mkumbwa wakati wa mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa dawa, Vifaa tiba na Vitendanishi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro yaliyofanyika  Ukumbi wa Bwalo la Umwema katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



Bi. Sonia amesema lengo la kukasimu mamlaka hayo, pamoja na kuongeza Ushirikiano baina ya pande hizo mbili ni kuwajengea uwezo Wakaguzi hao katika kudhibiti Ubora wa Dawa na Vifaa tiba ili kulinda Afya za Watumiaji kwa kuwa wao wako Kitaifa na Kikanda na kwamba peke yao hawawezi kufika kila mahali kufanya shuguli hizo za ukaguzi wa dawa.

“kwa sababu TMDA iko Kitaifa na katika Ofisi za Kanda hatuwezi kufika katika kila Halmashauri na kuwa na Watumishi wetu” alibainisha  Sonia Mkumbwa

Aidha, amesema lengo kubwa ni kuwasogezea wananchi huduma hiyo ukilinganisha ukubwa  wa maeneo ya nchi hii na uchache wa watumisjhi wa TMDA hapa nchini ambao hawazidi 270 na hivyo ili kuongeza ufanisi zaidi wamefikia hatua ya kukasim Mamlaka yao kwa watumishi wa Halmashauri.


Afisa Mifugo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro Dkt. Gasper Msimbe akiwa katika mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa dawa,vifaa tiba na vitendanishi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro yaliyofunguliwa Juni 6 Mwaka huu.


Hata hivyo, Sonia amesema wakiwa katika kikao hicho, washiriki watapewa miongozo mbalimbali inayohusu utunzaji na usambazaji sahihi wa bidhaa hizo za Afya zikiwemo dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi namna ya kuziharibu mara baada ya kupoteza ubora unaohitajika kwa Binadamu.

Akifungua Mafunzo hayo Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozaria Rwegasira pamoja na kushukuru TMDA kutao mafunzo kwa watalaamu hao amewataka TMDA awaendelee kuwajenge uwezo zaidi watalaam hao kwa kuwa Elimu haina mwisho na kwamba kadri watakavyojengewa uwezo ndivyo watakuwa na uwezo wa kudhibiti madhara makubwa kwa binadamu yatokanayo na kutumia dawa zisizo na ubora.


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira akizungumza na wakaguzi wa TMDA katika mkutano na wakaguzi wa dawa, Vifaa tiba na Vitendanishi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro, mkutano uliofanyika Juni 6 mwaka huu katika ukumbi wa Bwalo la Jkt Umwema.


Aidha Dkt. Rozaria amewataka washiriki ambao ndio wataalamu wa maabara, Wafamasia na waganga wa mifugo kufanya kazi kwa uaminifu na weledi zaidi ili kufikia malengo ya TMDA ya kukasimisha mamlaka yao Kwao kwa kulinda Afya za wananchi kwa kutoa huduma iliyo Bora na Salama.


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rozalia Rwegasira (wa kwanza kushoto) akiwa na Afisa Mifugo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  wa Morogoro Dkt. Gasper Msimbe pamoja na Meneja wa TMDA Kanda ya Kati Dkt. Sonia Mkumbwa.

Nao washiriki wa Mafunzo hayo akiwemo Felisia Mapunda ambaye ni Mfamasia wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga pamoja na kuishukuru Serikali kupitia TMDA kushiriki mafunzo hayo amebainisha kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kwenda kufanya kazi kwa weledi lakini zaidi kwenda kumlinda mwananchi kutopata dawa ambazo hazina ubora.


Picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo yaliyoandaliwa na TMDA yaliyofanyika ukumbi wa JKT Bwalo la Umwema Juni 6 mwaka huu Mkoani Morogoro.


MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.