• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Tume ya kuboresha Taasisi za Haki Jinai yapiga hodi Morogoro, wadau watoa mapendekezo.

Posted on: October 28th, 2023

Tume ya kuangalia namna ya kubororesha Taasisi za Haki Jinai hapa nchini ambayo iliundwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kukusanya maoni juu ya kuboresha taasisi hizo imefanya kongamano lake Mkoani Morogoro na kukutana na wadau mbalimbali ili kupata maoni yao juu ya mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo kwa Mhe. Rais.

Hawa ni Wajumbe wa Tume ya kuboresha Taasisi za Haki Jinai wa kwanza kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu IGP Ernest Mangu, Bw. Omary Issa, Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu IGP Said Mwema wakati wa Kongamano la haki jinai.

Tume hiyo imefanya Kongamano hilo Oktoba 27, 2023 lililolenga kukusanya maoni juu ya mapendekezo ya kuboresha taasisi za haki jinai hapa nchini, kongamano ambalo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Mount Uluguru uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akibainisha mapendekezo yaliyotolewa na Tume hiyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu hapa nchini IGP Ernest Mangu amesema miongoni mwa mapendekezo waliyoyatoa ni pamoja na kuandaliwa mkakati wa kitaifa wa kubaini na kuzuia uhalifu, matumizi ya Tehama kwa taaisi zinazohusika na mifumo ya haki jinai, ukamataji wa waharifu kuachiwa jeshi la polisi, uwepo wa matumizi mabaya ya madaraka kwa baadhi ya watendaji wa Serikali na kuundwa kwa chombo cha kitaifa cha upelelezi.

Naye, Bw. Omary Issa ambaye ni Mjumbe wa Kamati hiyo amesema tume hiyo imekasimiwa madaraka na kuwa Kamati ya kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo kwa taasisi zenye mifumo ya haki jinai ambapo zinakadiliwa kufikia taasisi 18. Aidha, ameongeza kuwa baadhi ya mapendekezo hayo yatachukua muda mrefu katika utekelezaji wake na mengine yameshaanza kufanyiwa kazi. 

Hawa ni baadhi ya wajumbe wa Tume ya kuboresha Taasisi za Haki Jinai kulia ni Bw. Omary Issa na mwengine ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu IGP Said Mwema wakiwa kwenye Kongamano la haki jinai.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima, ameishukuru Tume hiyo kwa umahili wao wa kufanya kazi, huku akimpongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwateua watu wajumbe makini na kwamba kwa uthubutu na utendaji wao anaamini nia aliyoikusudia itatimia.

Nao baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Morogoro Ndg. Fikiri Juma amependekeza kubadilisha jina la Magereza na kuitwa chuo cha mafunzo ili wafungwa wapate mafunzo badala ya mateso. Aidha, amependekeza kuwa  Taasisi za kijeshi ziajiri Wataalam wa lugha ya alama ili kuwasaidia watanzania wenye matatizo ya kusikia kuweza kuwasiliana na wenzao kwa urahisi.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Morogoro Ndg. Fikiri Juma akitoa maoni wakati wa Kongamano la haki jinai.

Tume ya kuboresha haki jinai iliundwa kwa lengo la kuangalia mfumo wa haki jinai na taasisi zake ili kubaini mapungufu yake na kisha kuja na mapendekezo ya kuuboresha.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.