• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Tunataka tuifanye Morogoro liwe Jiji - RC Malima.

Posted on: July 3rd, 2024

Serikali Mkoani Morogoro ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima imedhamiria na inaendelea kuweka mikakati na mipango madhubuti kuhakikisha Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inakuwa miongoni mwa Miji mikubwa hapa Nchni.

Hayo yamebainishwa  Julai 2, 2024 na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa kikao Maalum cha Baraza la Madiwani  la Halmashauri hiyo cha kujadili  hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika mkoani humo.

Mhe. Malima amesema kupitia ujio wa reli ya kisasa ya mwendo kasi (SGR) inakuwa chachu ya maendeleo katika Mkoa huo na itachangia kwa vikubwa  Mkoa wa Morogoro kuwa jiji  kwa sababu ya uwepo wa wasafiri wengi wanaopita mkoani humo ambao wataongeza mzunguko wa fedha na Halmashauri kujipatia mapato ya kutosha.

"...sasa nyie mkitaka kujiita city village ni nyie lakini mimi nataka Morogoro iitwe city council.." amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amesema, Halmashauri hiyo haiwezi kuwa jiji kama ukusanyaji wa mapato ya ndani ni hafifu, pamoja na kuipongeza kuwa ndiyo Halmashauri inayoongoza kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani kati ya Halmashauri zote za Mkoa huo, bado ameitaka Halmashauri hiyo kuweka mikakati ya kuongeza ukusanyaji wa  mapato ya ndani kwa dhamira ya kukidhi moja ya vigezo vya kuwa jiji lakini pia kuwaletea wananchi maendeleo.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amesema anasikitika sana kuona Halmashauri ya manispaa ya Morogoro inakuwa na mazingira machafu muda wote, likiwemo soka la Mawenzi. hivyo, amewataka watendaji kufanya jitihada na kutafuta mbinu mbadala za kutatua changamoto hiyo ya kuusafisha mji huo  ili kuhakikisha mazingira ya manispaa hiyo yanakuwa safi.

Sanjari na hilo  Dkt. Mussa amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanakusanya kodi kwa wafanyabiashara wote wa mji huo, kwani kuna kila dalili za manispaa hiyo kutokusanya kodi kwa baadhi ya wafanyabiashara au kama kodi hiyo inakusanywa basi haiingizwi kwenye mifuko ya Serikali.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa amesema Halmashauri hiyo ina mpango wa kuupanga mji huo kuwa wa kisasa zaidi ikiwa ni pamoja na kuondoa vibanda ambavyo vimekaa maeneo yasiyo sahihi, kupanga biashara mahali panapo stahili na kutoza faini kwa wale watakaobainika kuchafua mazingira ya manispaa hiyo ili kuhakikisha usafi unazingatiwa  hususan kipindi hiki cha kujipanga kuelekea Morogoro kuitwa Jiji.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.