• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Twaha Kiduku arejea kwa kishindo Morogoro.

Posted on: November 1st, 2020

Maelfu ya Wananchi Mkoani Morogoro wamejitokeza kumpokea Mwanamasumbwi  Twaha Ramadhani Kiduku wakati akirejea kutoka Jijini Dar es Salaam baada ya kuibuka Mshindi kwenye   pambano lililofanyika Oktoba 30 Mwaka huu dhidi ya Bondia mwenzake kutoka Thailand.

Mapokezi hayo yamefanyika Novemba mosi Mwaka huu ambapo  mapokezi hayo yalianzia Nanene katika Maispaa ya Morogoro kuelekea nyumbani kwake huku Umati wa watu ukifurika kumuunga Mkono na kumpongeza kwa ushindi huo.

Kiduku aliibuka Mshindi katika raundi ya saba baada ya kumchakaza bondia Sirimongkhon Lamthuam katika pambano la raundi 10 uzito wa Super Welter lililofanyika ukumbi wa PTA Saba Saba, barabara ya Kilwa, Jijini Dar es Salaam na kujinyakulia ubingwa wa Kimataifa wa WPC hivyo kuvunja rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kuchukua ubingwa huo.

Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kuwasiri Mkoani Morogoro, Kiduku amesema hajaridhika na ushindi huo hivyo ataendelea kupambana ili kuwa bingwa ndani na Nje ya Nchi huku akiutangaza Mkoa wa Morogoro na Tanzania kwa ujumla.

“Mimi nawaambia tu …..Bendera chuma Mlingoti chuma, bado sijaridhika na mapambano haya nahitaji kufanya vizuri zaidi ndani na nje ya Nchi show show” alisema Kiduku.

Aidha, bondia huyo ametoa shukrani kwa Wananchi wote wa Mkoa wa Morogoro waliojitokeza kumpokea na wadau mbalimbali waliomuunga Mkoano wakiwemo Babu Tale, Mbaraka Ali Said, Rashid Bodaboda na wengine ambao kwa namna moja au nyingine wamechangia kuibuka mshindi wa pambano hilo.

Kwa upande wake Kocha Charles Mbwana ametoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare na viongozi waandamizi wake kwa kuwakaribisha vizuri, kuwatendea haki Mabondia na kuwatuma kuleta Ubingwa katika Mkoa huo.

Naye Kaimu Afisa Michezo Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Afisa Vijana Mkoa wa Morogoro Bi. Winnifrida Madeba, ametoa shukrani kwa wadau waliojitokeza  kumuunga mkono mwanamasumbwi huyo kuanzia maandalizi yake, wakati wa pambano hadi ubigwa unapatikana pamoja na mapokezi yake hapa Mkoani.

Pamoja na shukrani hizo Bi. Winnifrida ametoa ombi kwa wadau wa Michezo na wengine katika Mkoa wa Morogoro kujitokeza kushiriki katika  Michezo mbalimbali na kuwasaidia Vijana kwani wao peke yao hawawezi kuleta mafanikio, hivyo serikali itaendelea kuunga mkono jitihada zao katika kuboresha Michezo Mkoani hapa ili vijana waweze kufikia ndoto zao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya Wananchi waliohudhuria kumpokea Mwanamasumbwi huyo akiwemo Shaabani Mahamud, amesema Kiduku amefanya maajabu ambayo hayajawahi kufanyika Mkoani hapa na   ameutangaza vizuri Mkoa huu huku akitaka pambano kati ya Twaha na Mwakinyo.

Hii ni mara ya Pili kwa Mwanamasumbwi Twaha Kiduku kurejea na ubingwa Mkoani Morogoro ambapo mara ya kwanza alishinda shindano la kitaifa na sasa ameshinda shindano la Kimataifa.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.