• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Twaha Kiduku atoa siri ya ushindi wake, amtaja JPM

Posted on: November 3rd, 2020


Na Andrew Chimesela, Morogoro.

Mwanamasumbwi wa kimataifa Twaha Kiduku ametaja siri  ya ushindi na mafanikio yake kuwa ni Morali aliyopewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata ole Sanare huku akidai kuwa msingi mkubwa wa mafanikio hayo ni uwepo wa amani hapa nchini chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Twaha Kiduku amesema hayo Novemba 3 Mwaka huu alipokwenda Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kutoa shukrani zake kwa ushirikianao waliompa kabla na baada ya pambano lake la kimataifa la Oktoba 30 kati yake na Sirimongkhon Lamthuam kutoka Thailand ambalo lililomuwezesha kupata ushindi wa  Technical Knock Out (TKO).

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini hapo Twaha kiduku ametoa shukrani kwa Loata Ole Sanare Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Katibu Tawala wa Mkoa huo Emmanuel Kalobelo na viongozi wengine kwa kumuunga mkono kabla na baada ya pambano lake.

“Ushindi huu umetokana na nguvu nyingi sana za Mkuu wangu wa Mkoa kunipa moyo na Viongozi wote wa Mkoa wa Morogoro, kwasababu najua pindi nilipokuwa naenda kuingia ulingoni Mkuu wa Mkoa wangu ananiangalia, RAS wangu wa morogoro  ananiangalia na viongozi wote, pia Tanzania nzima inaniangalia hivyo nikasema siwezi kuuangusha Mkoa wangu na watanzania kwa ujumla” Alisema Kiduku.

Hata hivyo, Twaha Kiduku aliweka bayana kwa watanzania kuwa siri ya ushindi huo pia ni AMANI iliyopo hapa nchini ndiyo inayopelekea kila mtu anaendelea na shughuli zake na amani hiyo inatokana na uongozi madhubuti wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli  wa Tanzania.

”Pia namshukuru sana Rais wetu John Pombe Magufuli kwa kuweka viongozi kuwa salama kwasababu laiti kama uongozi wake usingelikuwa imara sidhani kama pambano letu lingefanyika vizuri” Alisema Kiduku

Aidha, Kiduku amesema Desemba 26 Mwaka huu anatarajia kushiriki pambano la usiku wa Mabingwa wa kimataifa ambalo linahusisha Watanzania na mabondia kutoka Nje ya Nchi litakalofanyika Jijini Dar Es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amesema Mkoa wa Morogoro umepanga kuandaa miundombinu inayojitosheleza itayowezesha kila mwenye kipaji cha Mchezo wowote kushiriki na kusaidiwa katika kukuza kupaji hicho.

Sambamba na hilo, ametoa pongezi kwa Mwanamasumbwi huyo kwa kutimiza ahadi yake ya kurejea na ubingwa wa Kimataifa  katika Mkoa wake kama ambavyo alikuwa amemuahidi Oktoba 27 Mwaka huu  kabla ya kuelekea Jijini Dar es salaam kwa ajili ya pambano hilo.

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo Mkoani humo Mhandisi Emmanuel Kalobelo ametoa agizo kwa Halmashauri zote Mkoani humo kuandaa miundombinu kwa ajili ya Michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Boxing.



Mhandisi huyo amesema Mkoa wa Morogoro umejipanga vizuri kuipa kiupaumbele Michezo huku akiwasihi vijana wenye vipaji katika mchezo wowote kujitokeza ili kutambua vipaji vyao na kuweza kuwasaidia wanamichezo wengine ambao hawafahamiki.

Pia, Mhandisi huyo ametoa ombi kwa Uongozi wa Twaha Kiduku kuunda Taasisi itakayo ongoza na kuratibu kazi anazozifanya mwanamasumbwi huyo ili kutunza rekodi ya matukio yote anayoyafanya na kutambulika kwa rasilimali watu ambao wanamuunga Mkono katika kazi zake.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.