• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Twaha Ramadhan (Kiduku) aagwa, atakiwa kutangaza vivutio.

Posted on: August 18th, 2021

Mwanamasumbwi maarufu wa ngumi za kulipwa Mkoani Morogoro Twaha Ramadhani almaarufu kama Twaha Kiduku ameagwa leo rasmi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuelekea kwenye pambano lake la ngumi baina yake na Dulla Mbabe linalotarajiwa kufanyika Agosti 20 mwaka huu Jijini Dar es  Salaam.

Waliomuaga katika hafla hiyo fupi leo Agosti, 18 mwaka huu ni pamoja na mashabiki wa Twaha Kiduku, Menejimenti ya Kiduku pamoja na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Martine Shigela.

Akitoa nasaha kwa Mwanamasumbwi huyo, Bi. Mariam Mtunguja ambaye pia ni Mwenyekiti wa Michezo Mkoani humo, amemtaka Mwanamasumbwi Twaha Kiduku kutumia nafasi aliyonayo kutangaza vivutio mbalimbali vilivyopo katika Mkoa wa morogoro ili kuwavutia watalii wengi kuja nchini.

Amesema Mkoa wa Morogoro una vivutio vingi ambavyo watalii kutoka nje na ndani ya nchi wangelipenda kuviona zikiwemo mbuga za wanyama, mradi wa bwawa la Mwalimu Nyerere, mradi wa SGR na milima ya udzungwa.

‘’… Lakini Morogoro kuna fursa chungu nzima za uzalishaji, kwa hiyo wewe usiangalie  ngumi tu, wewe utakachokizungumza  wanakiamini, nikuombe sana utusaidie kuubeba Mkoa wa Morogoro kwa kututangazia vivutio vya utalii na fursa zilizopo katika Mkoa wa Morogoro…’’ ….amesema Bi. Mariam.

Kwa upande wake Twaha kiduku amemhakikishia Katibu Tawala huyo, Mkuu wa Mkoa Martine Shigela pamoja na mashabiki wote wa ngumi Mkoa wa Morogoro na Mikoa mingine kupata ushindi katika pambano hilo na kurudi na ushindi.

Amesema ushindi huo utatokana na hamasa ya pamoja aliyopewa na viongozi mbalimbali wa ndani ya Mkoa huo ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Mratibu wake Afisa Michezo Bi. Grace Njau.

Naye, Afisa Michezo Mkoa wa Morogoro Bi. Grace Njau amewahakikishia wanamasumbwi wanaochipukia Mkoani humo kujitokeza kwenye mchezo huo kwani tayari Mkoa unaendelea kuwawekea mazingira mazuri ya kufanyia mazoezi ya ngumi ikiwa ni pamoja na eneo la DDC.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.