• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Ukusanyaji mapato wafikia trilioni 7.5 sekta ya utalii

Posted on: January 25th, 2025

Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Gerson Msingwa amesema kumekuwa na ongezeko la ukusanyaji wa mapato katika sekta ya utalii kufikia trilioni 7.5 kwa mwaka 2023/2024 ambapo hapo awali mapato hayo yaliishia trilioni 2 hadi 3 pekee.

Msigwa amebainisha hayo Januari 25, Mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa habari ndani ya hifadhi ya Taifa ya Mikumi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Akifafanua zaidi, Msigwa amesema mapato hayo yametokana na ongezeko la watalii katika hifadhi za Taifa kutoka watalii 1,618,538 mwaka 2022/2023 hadi watalii 1,863,108 mwaka 2023/2024, hivyo kutokana na uwepo wa ubora wa miundombinu hususan barabara, Viwanja vya ndege na michezo na kumechochea ongezeko la mapato hapa nchini.

"...Mapato yetu yameongezeka sana sasa hivi tunazungumza mapato ya takribani trilioni 7.5 ambayo tumeyapata kupitia watalii wanaokuja kwenye hifadhi zetu..."
amesema Msigwa.


Aidha, Msigwa amesema Serikali imejipanga kukusanya kiasi cha Tsh. Bil. 430.9 Kupitia TANAPA katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 lakini hadi kufikia Juni hadi Disemba zimekusanywa Tsh. bil. 325.1

Katika hatua nyingine, Gerson Msingwa amesema serikali imefanikiwa kutatua migogoro mbalimbali iliyokuwa ikiikumba sekta ya utalii ukiwemo mgogoro wa hifadhi ya Tarangire na kijiji cha Kimotoroki.

Migogoro mingine ni pamoja na ile ya hifadhi ya Serengeti na Vijiji saba vya Wilaya ya Serengeti, hifadhi ya Ruaha na Vijiji vya Mbalali, hifadhi ya Taifa ya Milima ya Mahale na Kijiji cha Kalilani huku serikali ikiendelea kuelimisha wananchi kuondokana na migogoro isiyo ya lazima kwenye maeneo ya hifadhi.

Sambamba na hayo, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kusimamia na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika kushughulikia shughuli za kihifadhi, ukusanyaji wa mapato, utangazaji wa utalii na fursa za nje ya nchi ili kukuza kipato cha Taifa.

Pia, Katibu Mkuu huyo amesema Serikali kupitia TANAPA imefanya uwekezaji na kuimarisha uhifadhi wa wanyama pori na makazi ya wanyama kwa kuimarisha ulinzi na usalama wa kiteknolojia na kufuatilia mienendo ya wanyama waliopo hatarini kutoweka wakiwemo Faru, Sokwe na Mbwamwitu ili rasilimali ziweze kuwa endelevu kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.