• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

UMOJA NA MSHIKAMANO NDIYO NGUZO, MAFANIKIO YA MKOA WA MOROGORO.

Posted on: October 7th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima amesema ili Mkoa huo uweze kuyafikia mafanikio inahitaji Viongozi kuwa na umoja na mshikamano, sauti moja, uzalendo, upendo baina yao ili kuhakikisha kuwa wananchi wa Mkoa huo wanapata maendeleo.

Mhe. Adam Malima ameyasema hayo Oktoba 6 mwaka huu kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha ualimu cha Morogoro kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Mkoa wa Morogoro una fursa nyingi za kiuchumi kwenye kilimo, mifugo, na utalii ambazo zikiratibiwa na kusimamiwa vizuri Mkoa utapata mafanikio kuliko Mikoa mingine hapa nchini, hivyo amewataka viongozi hao kubadilisha mitazamo yao na kuupa kipaumbele Mkoa ili uweze kufanikiwa.

“...tunahitaji Morogoro tofauti, tunataka kuitoa Morogoro hapa ilipo sasa, tunahitaji kuibadilisha Morogoro bila kuchapana viboko aone tu kwamba ni sehemu ya majukumu yake...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Malima ameziagiza Halmashauri za Mkoa huo kuendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kufikia shilingi Bilioni 60 kwa mwaka wa fedha 2024/2025, hata hivyo amezitaka Halmashauri hizo kubainisha maeneo ya uwekezaji pamoja na kuboresha miundombinu ili kuvutia wawekezaji.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amemkataa Meneja wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushindwa kusimamia miradi ya usambazaji umeme katika Vijiji vingi vya Mkoa huo huku akimrudisha makao makuu Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) wa Mkoa kwa kushindwa kuhudhuria bila sababu vikao muhimu vya kujadili masuala ya kimaendeleo ya Mkoa ambavyo vinalenga kutatua kero za wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Kilosa Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwenyekiti wa Wabunge Mkoani humo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa nia yake njema ya kutaka Mkoa huo kufikia mafanikio yanayotarajiwa na wanamorogoro na watanznia wote huku akiwaomba viongozi kushirikana kubadilisha mitazamo ya wanamorogoro waweze kufikirie maendeleo zaidi. 

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Sebastian Waryuba ambaye pia ni mwenyekiti wa Wakuu wa wilya za mkoa huo kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya wa Mkoa huo amemshukuru Mhe. Adam Malima kwa kuja na mipango thabiti ya kuuendeleza Mkoa huku akikiri kuwa watampa ushirikiano na kuyafanyia kazi maelekezo yaliyotolewa ili kufainikisha nia yake ya kuupatia maendeleo Mkoani huo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.