• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Unyanyapaa ni mzizi wa maambukizi ya VVU/UKIMWI, Jamii yashauriwa kuondokana nao.

Posted on: November 28th, 2023

Wataalam wa masuala ya VVU na UKIMWI wamebainisha kuwa unyanyapaa kwa watu waishio na VVU ni miongoni mwa sababu zinazopelekea kuongezeka kwa maambukizi hayo, hivyo wameishauri jamii kuachana na tabia ya Kuwanyanyapaa watu waishio na VVU.

Hayo yamebainishwa Novemba 28, 2023 na Mratibu wa masuala ya Jinsia kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI – TACAIDS Bi. Priscilla Nalitolela wakati wa mahojiano na mwandishi wa Habari hizi kwenye Kijiji cha Jamii ikiwa ni muendelezo wa Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani 2023.

Bi. Priscilla amesema kuwa unyanyapaa ni hali ya kumtenga mtu kutokana na hali yake kiuchumi, kiafya na kielimu. Aidha, ameongeza kuwa unyanyapaa kwa watu wenye VVU husababisha kuongezeka kwa maambukizi kwa sababu ya watu waishio na virusi wanakuwa wasiri kutowaambia watu wengine hali zao kuhofia kutengwa.

Mratibu huyo amebainisha madhara ya unyanyapaa yakiwemo kuharibu utaratibu wa dawa kwa watu waishio na VVU, kuongezeka kwa maambukizi kutokana na watu wenye VVU kuwa wasiri katika jamii.

Pamoja na madhara hayo Bi. Priscilla amesema unyanyapaa upo katika ngazi mbalimbali ikiwemo unyanyapaa binafsi, kaya/familia na unyanyapaa ndani ya jamii.

Katika hatua nyingine Bi. Priscilla ametoa wito kwa Vijana kujiamini kwenda kupima kujua hali zao za kiafya na kuanza kutumia dawa za kufubaza VVU – ARV kwa wale watakaobainika kuwa na maambukizi hayo.

Nao baadhi ya vijana waliotembelea na kupata elimu kwenye Kijiji hicho cha jamii akiwemo Bw. Kelvin Mrekoni amesema uwepo wa Kijiji cha Jamii kimemsaidia kufahamu mbinu mbalimbali za kudhibiti maambukizi ya VVU na UKIMWI katika jamii huku akiwashauri vijana wengine kuwa wawazi ili kudhibiti maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI.

Bw. Lyassa Lyassa ni mmoja wa watu waishio na VVU ametumia fursa hiyo kuwashauri vijana kwenda kupima ili kubaini hali zao za kiafya kwa kufanya hivyo kutatimiza lengo la Serikali la kufikia Sifuri tatu ifikapo 2025 yaani kuwa na asilimia sifuri ya maambukizi mapya, kuwa na asilimia sifuri ya vifo vinavyotokana na VVU na UKIMWI na kuwa na asilimia sifuri ya unyanyapaa kwa watu waishio na VVU.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.