• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

UPATIKANAJI WA MBEGU BORA ZA MAZAO YA ALIZETI NA MCHIKICHI SULUHISHO LA MAFUTA YA KULA NCHINI.

Posted on: June 1st, 2022

Upatikanaji wa mbegu bora za mazao ya alizeti na mchikichi na uwezeshaji wa wananchi katika kilimo cha mazao hayo kwa njia ya mikopo nafuu na ruzuku mbalimbali za pembejeo ni suluhisho la uhaba wa mafuta ya kula hapa nchini.




Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo na Umwagiliaji Hussein Bashe kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa Sekta ya mafuta ya kula uliofanyika Mei 31 Mwaka huu katika Hoteli ya Morena iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akihutubia Mkutano wa Wadau wa Sekta ya mafuta ya kula hapa nchini Mei 31 Mwaka huu uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Moreni uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.





Martine Shigela amebainisha kuwa Serikali kwa kutambua uhaba wa mafuta ya kula hapa nchini, pamoja na kufanya jitihada mbalimbali ili upatikanaji wake uwe wa bei nafuu imeendelea kushawishi uwekezaji na wawekezaji katika kilimo cha michikichi na alizeti ili kufikia malengo hayo ya Taifa.

“Zao la alizeti ni miongoni mwa mazao ya kimkakati, kwa hiyo ni miongoni mwa mazao ambayo tukiwekeza vizuri tutaweza kufikia malengo tunayoyatarajia na ndio maana mwaka jana tumesambaza mbegu bure kwa wakulima wetu kama motisha” amebainisha Shigela.





Katika hatua nyingine kupitia Hotuba hiyo Mkuu huyo wa Mkoa ameweka wazi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetenga bajeti zaidi ya shilingi bilioni 150 kwa ajili ya pembejeo za ruzuku ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kilimo cha mazao yakiwemo ufuta, alizeti na michikichi ili kuhakikisha changamoto ya mafuta ya kula inafikia mwisho.



Baadhi ya washiriki wa mkutano wa wadau wa Sekta ya mafuta ya kula hapa nchini wakishiriki ufunguzi wa mkutano huo uliofunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela Mei 31 Mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Morena uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



Aidha ndugu Beatus Malema ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Uendelezaji mazao, masuala ya pembejeo na Ushirika kutoka Wizara ya Kilimo, amesema kuwa badala ya kutumia bilioni 400 kwa ajili ya kuagiza mafuta nje ya nchi ni vema kama taifa kwa kushirikiana na wadau kuendeleza kilimo cha zao la mchikichi na alizeti ili kuondoa kabisa tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula hapa nchini.





Kwa upande wake Bw. Henry Mariale ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha wakulima wa zao la Alizeti ameiomba Serikali kusaidia mbegu bora za alizeti na zinazoweza kutosheleza kwa wakulima hao, ambapo kama chama wamejipanga kuleta hamasa kwa kila kaya wanaojihusisha na kilimo cha alizeti kulima heka mbili ili kuweza kusaidia upatikanaji endelevu wa mafuta yatokanayo na zao hilo hapa nchini.




Naye Bw. Ringo Ringo ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha wasindika Mafuta Tanzania (TASUBA) amebainisha kuwa changamoto ya ukosefu wa mafuta hapa nchini umechagizwa kwa kiasi kikubwa na uhaba wa upatikanaji wa alizeti, kwani viwanda vya usindikaji vinapokea mali ghafi hiyo kwa uchache zaidi ukilinganisha na mahitaji halisi.




Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano wa wadau wa Sekta ya mafuta ya kula baada ya ufunguzi wa mkutano huo Mei 31 Mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Morena uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.



MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.