• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

UTITIRI WA KODI CHANGAMOTO KWA WAFANYABIASHARA.

Posted on: January 23rd, 2025



Imeelezwa kuwa utitiri wa Kodi kwa wafanyabiashara ni moja ya changamoto kubwa inayolalamikiwa na kundi hilo na kwamba jambo hilo si tu linadhohofisha maendeleo ya wafanyabiashara hao kuendesha biashara zao lakini pia linaikosesha Serikali kupata kodi inayostahili.

Hayo yamebainishwa Januari 22, 2025 na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Maboresho ya kodi Balozi Mwanaid  Maajar wakati wa kikao cha Tume hiyo kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Mbaraka Mwinshehe Manispaa ya Morogoro na kushirikisha wafanyabiashara mbalimbali wa kodi Mkoani humo  kwa lengo la kukusanya maoni, changamoto na mapendekezo ili Serikali iweze kuboresha ukusanyaji wa kodi hizo.

Balozi Mwanaid amesema, kilio cha wengi ni utitiri wa kodi unaotokana na uchache wa walipa kodi huku Mamlaka husika zikiwa zinaelekeza nguvu zake za kudai kodi sehemu mojaama chache ili kupata kodi jambo ambalo linamrudisha nyuma mfanyabiashara kwa sababu ya kulipa kodi nyingi.

".. Utitiri wa kodi na watozaji wenyewe imejirudia mara nyingi kwamba wanafika watozaji wapatao hata wa tano kwa siku na bila mtu kujua.." amesema Balozi Mwanaid.

Katika hatua nyingine Balozi huyo ameeleza lengo la Tume hiyo kuwa imelenga kupokea malalamiko, changamoto na mapendekezo ili kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kuangalia namna ya kurahisisha utaratibu wa wafanyabiashara kupata leseni, kulipa tozo na kulipa kodi kwa urahisi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Morogoro Bi. Beatrice Njawa amesema katika eneo muhimu sana katika kuboresha mazingira ya biashara hapa Nchini ni kuangalia suala la wingi wa kodi ambalo linaweza  kuwavutia wawekezaji wengi, hivyo ameiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kushirikiana katika kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara  juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa  Chemba ya Wafanyabiashara na Kilimo Mkoa wa Morogoro (TCIA) Mwadhine Mnyanza amesema wafanyabiashara hukumbana na changamoto mbalimbali zikiwemo wingi wa kodi, kodi kubwa hasa katika sekta zinazokuwa kibiashara jambo linalopelekea wafanyabiashara kufikia hatua ya kukwepa kodi.

Naye Katibu wa Chama Cha Walimu (WCT) manispaa ya morogoro Bw. George Lukoa amesema, moja ya kero kubwa wanayokumbana nayo wafanyakazi wa Umma hususan Walimu ni juu ya kodi ya makato (pay as you earn) kuwa kubwa jambo ambalo linapelekea mtumishi huyo kupata mshahara mdogo  usiokidhi mahitaji hivyo ameiomba Serikali kuangalia upya suala hilo ili kupunguza kodi hiyo.

Katika hatua nyingine Bi. Redempta Mushi akieleza changamoto wanayokumbana nayo pindi wanapofanya biashara zao Zanzibar amesema, Mfanyabiashara kutoka Tanzania bara anatakiwa alipe kodi anapopeleka biashara zake zanzibar lakini mfanyabiashara kutoka Zanzibar halipi kodi jambo ambalo amesema inafaa liangaliwe ili kuweka uwiano kwa pande hizo mbili.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bi. Zahara Michuzi ameunga mkono hoja ya Serikali kuangalia kwa jicho la huruma mishahara ya wafanyakazi kwani amesema makato ni makubwa mno na mishahara haiongezeki jambo ambalo linapelekea umasikini kwa watumishi hao.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.