• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

VIJANA MKOANI MOROGORO KUNUFAIKA NA MRADI WA KIJANA NAHODHA.

Posted on: April 15th, 2023

Vijana Mkoani Morogoro wanatarajia kunufaika kupata masomo ya Elimu ya Sekondari huria (QT) na mafunzo ya ufundi stadi kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 kwa ufadhili kutoka Serikali ya Watu wa Marekani kupitia Mradi wa USAID KIJANA NAHODHA.

Kwa mujibu wa Meneja wa Mradi wa USAID KIJANA NAHODHA Bw. Samuel Chambi, amesema  ufadhili huo kwa vijana watakao kidhi  vigezo vilivyowekwa utajumuisha ada, chakula na usafiri kwa vijana wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 25.

habari hiyo njema kwa vijana imebainishwa  wakati wa mafunzo ya uhamasishaji wa mradi huo ngazi ya jamii Mkoani Morogoro yaliyotolewa kwa Halmashauri mbili za Morogoro DC na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mafunzo hayo ya kutambulisha mradi huo yametolewa kwa Wadau mbalimbali wakiwemo Wahe. Madiwani wa kutoka kata zilizochaguliwa kunufaika na mradi huo kwa awamu hii ya kwanza, Maafisa elimu wa Kata husika pamoja na  Maafisa Maendeleo ya Jamii wa halmashauri nufaika.

Akifungua mafunzo hayo kwa  Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Aprili 14 mwaka huu katika hoteli ya Flomi, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Pascal Kihanga amekiri kuwa kuanzishwa kwa mradi wa USAID KIJANA NAHODHA katika Manispaa hiyo utasaidia vijana wengi kujikwamua katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Wakizungumzia manufaa ya mradi huo siku ya kwanza ya kuutambulisha, wajumbe wa mafunzo hayo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Lucas Lemomo amesema itawarahisishia wasichana na wavulana ambao walikatisha masomo yao kwa sababu mbalimbali kuendelea na masomo huku wakiendelea  na shughuli zao nyingine za Uzalishaji.

Ameongeza kuwa mradi huo utawasaidia vijana hao kupata ujuzi lakini zaidi kufikia malengo yao ambayo walishakata tamaa kuyafikia.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo Bi. Frola Mwambele amesema mafunzo hayo yatawafikia vijana wengi ambao awali walikuwa hawapati fursa ya kufikiwa na miradi mbalimbali hivyo ni fursa kwa kwao kubadilisha maisha kupitia mradi huo.

Mradi huo wa miaka mitano ambao ulianza Septemba 2022 na utakamilika 2026 unatekelezwa kwa Mikoa yote ya Tanzania Visiwani na kwa Tanzania Bara utatekelezwa kwa mikoa miwili ya Morogoro na Dar es salaam ukilenga kuwafikia na kuwanufaisha jumla ya vijana 45,000 wa kutoka Maeneo hayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.