• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Vijana watakiwa kujitokeza kupima VVU

Posted on: December 23rd, 2023


Wito umetolewa kwa vijana wa umri wa kati ya miaka 15 hadi 24 kujitokeza kwa wingi  kupima afya zao ili kukabiliana na  ongezeko la maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na VVU hapa nchini 

Wito huo umetolewa Novemba 26 mwaka huu na Naibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu Mhe. Patrobas Katambi kwenye kongamano la Vijana la Kisayansi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Morena.

Mhe. Patrobas Katambi amesema kuwa utafiti wa viashiria vya UKIMWI nchini uliofanyika 2016/2017 unaonesha kuwa kundi la vijana walio kati ya umri wa miaka 15 hadi 24 hawajui hali zao za maambukizi ukilinganisha na  makundi mengine hususan kundi la watu wazima.

“...natoa rai kwa vijana wote nchini kujitokeza kwa wingi katika huduma za upimaji VVU kwa hiari zinazotolewa sehemu mbalimbali hapa nchini...” amesema Naibu Waziri Patrobas Katambi. 

Aidha, amesema kuwa katika kuelekea lengo la sifuri ya maambukizi mapya, kutokana na jitihada mbalimbali za mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, maambukizi mapya yameendelea kushuka mwaka hadi mwaka ambapo watu 54000 waliambukizwa VVU mwaka 2021.

Sambamba na hilo, Naibu Wazri huyo amewaasa vijana kuwa na mitazamo chanya na kuwa na malengo madhubuti ya kufanya mambo kulingana na mazingira na jamii wanamoishi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Vijana Wanaoishi na VVU Bi. Pudensia Mbwiliza amesema nguvu kubwa inahitajika kuwasukuma Vijana ili waweze kubadilika kutokana na kuwa na mwitikio mdogo kwenye masuala ya VVU na UKIMWI huku akiwaasa vijana kushikamana ili kuhakikisha kuwa wanabadilika kwa lengo la kudhibiti maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI.

Naye mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la kudhibiti UKIMWI - UNAIDS Bi. Grace Mallya amesema mkakati wa kidunia wa kumaliza maambukizi ya UKIMWI ifikapo 2025 umeainisha kuwa asilimia 30 ya huduma zote za upimaji na tiba zifanywe na Vijana kutokana na  kundi hilo kuwa na idadi kubwa ya maambukizi mapya ya VVU, hivyo ametoa wito kwa wadau wa maendeleo kwa kushirikiana na Serikali kuwajengea uwezo Vijana ili kufikia malengo ya kumaliza maambukizi ya VVU na UKIMWI duniani.

Kongamalo hilo la Vijana la Kisayansi limewakutanisha vijana kutoka Vyuo vikuu, vya kati na Sekondari likilenga kubadilishana uzoefu na kupata uelewa juu ya kudhibiti na kujikinga maambukizi ya VVU na UKIMWI.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.