• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

VIJIJI 652 KATI YA 669 MKOANI MOROGORO VYAPATIWA UMEME

Posted on: October 4th, 2024

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuwapelekea umeme wananchi wa Vijiji 652 kati ya vijiji 669 vya Mkoa wa Morogoro kupitia Wakala wa Nishati ya Umeme Vijijini (REA) huku ikiahadi kukamilisha kupeleka nishati hiyo kwa vijiji 17 vilivyobaki ndani ya wiki tatu zijazo.

Hayo yamebainishwa Oktoba 4, Mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa kikao na viongozi wa REA kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kikiwa na lengo la kutathmini hatua za mradi ulipofikia na kumtambulisha mkandarasi mpya wa kampuni ya SINOTEC CO. LTD.

Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema, Mkoa huo una vijiji 669 ambapo vijiji vilivyofikiwa na nishati ya umeme ni 652 sawa na asilimia 97.5  huku vijiji 17 vilivyobaki vikiwa kwenye hatua za mwisho za ukamilishaji na kwamba vijiji hivyo vinatarajiwa kukamilika kupata umeme ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu.

“…nasema Morogoro ina vijiji 669 vilivyofikiwa  katika kipindi hiki ni vijiji 652 sawa na asilimia 97.5 huo ndio ukweli…” amesema Mhe. Adam Kighoma malima

Kutokana na mafanikio hayo, kiongozi huyo amesema, kwa sasa REA wameelekeza nguvu zao katika kuvipatia nishati ya umeme vitongoji 3,369 vya Mkoa huo huku vitongoji 1,655 tayari vimekwishapatiwa umeme sawa na asilimia 49.

Aidha, amesema vitongoji 455 vinatarajiwa kupatiwa umeme kwa kipindi cha miaka miwili na ndani ya hivyo vitongoji 289 mkandarasi anaendelea na ujenzi kupitia mradi wa ujazilizi (Densification IIB) na vitongoji 166 vitapatiwa umeme kupitia mkandarasi mpya aliyetambulishwa leo Oktoba 4, 2024.

Mhe. Malima ametumia fursa hiyo kuipongeza serikali  ya awamu ya sita kwa kuiwezesha REA kufanikisha mradi huo wa umeme ulioanza kutekelezwa kwa shilingi Bil. 2 pekee mwaka 2008 kwa nchi nzima na sasa serikali inatoa shilingi Bil. 154 kwa Mkoa huo pekee hivyo kuleta ufanisi kwa sekta nyingine za kijamii kama Elimu, Afya, na hata nyumba za ibada.

Sambamba na pongezi hizo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wadau mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa vijiji na vitongoji, watendaji wa kata na viongozi wengine kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi huyo ili kurahisisha utekelezaji wa mradi wenyewe.

Kwa upande wake, Mhandisi Mkuu wa Mkoa huo, Mhandisi Adam Abdulla kwa niaba ya Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro ameishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya mradi huo na kuahidi kuusimamia na kutoa ushirikiano kwa mkandarasi ili akamilishe kazi hiyo kwa wakati.

Naye, Msimamizi wa Miradi Kanda ya Kati Mhandisi Aneth Malingumu amesema, mradi huo ni maalum kwa kuwa usanifu wake umefanyika kupitia majimbo yote 11 ya Mkoa huo na kila jimbo litapata umeme katika vitongoji 15 likiwemo jimbo la Morogoro Mjini.

Mradi huu wa kufikisha nishati ya umeme vijijini unatekelezwa ndani ya miezi 24 na  mkandarasi atakayesimamia ni kutoka kampuni ya SINOTEC CO. LTD ambaye ametambulishwa leo Oktoba 4, Mwaka huu.


Mwisho



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.