• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Viongozi wa TASAF watakiwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa wanufaika.

Posted on: July 29th, 2023

Wajumbe wa kamati ya uongozi wa Taifa wa mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) wameridhika na utendaji kazi wa mradi wa mfuko huo na kuwataka viongozi wa TASAF kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa wananchi ili kuepuka fikra ambazo zinakwamisha maendeleo ya wananchi.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe akizungumza na wananchi.

Kauli hiyo imetolewa Julai 28, 2023 na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe wakati akiwa kwenye ziara yake ya siku moja pamoja na wajumbe wa kamati ya Uongozi wa Taifa wa TASAF  walipotembelea Kijiji cha Bamba kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mkoani Morogoro ikiwa na lengo la kuona jamii inavyonufaika na mradi huo.

Dkt. Maghembe ametoa kauli hiyo wakati akitoa ufafanuzi wa malalamiko kutoka kwa wanufaika wa mradi huo, baadhi ya malalamiko hayo ni pamoja na kutopewa taarifa sahihi na kwa wakati ya kununuliwa vifaa vya kusafishia barabara vikiwemo majembe ilihali vifaa hivyo tayari vilikuwa vimekwisha nunuliwa kwa ajili ya jamii hiyo.

Sambamba na hilo Dkt. Maghembe amewataka wananchi kutumia vizuri vifaa hivyo ili kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi huo na kupanua wigo wa kutoa huduma kwa wananchi.

"... Kwa hiyo niombe sana TASAF pamoja na Viongozi wote wa serikali za mitaa mliopo hapa tuwe na  mawasiliano mazuri na wananchi kwani tunavyo vikao vyetu vya ngazi ya kitongoji, Kijiji, kata, kamati za Afya na kamati za mazingira, tuvitumie kuwapa taarifa sahihi wananchi..." Amesema Dkt. Magembe.

Aidha, Dkt. Maghembe ameongeza kuwa Viongozi hao wanatakiwa kushirikiana na wananchi ili kuwaweka karibu na miradi ya maendeleo, hata hivyo amesema vikao vinavyofanyika vikiwemo vikao vya ngazi ya vitongoji, vijiji, Kamati za Afya, kamati za mazingira n.k. hivyo ni vikao vinavyotakiwa kutumika kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Maghembe amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Florence Mwaribewe kufanya marekebisho na kuongeza baadhi ya huduma zitakazotolewa katika kituo cha Afya cha Bamba ili kitoe huduma za uhakika kwa wananchi.

Pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa miundombinu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila akifafanua jambo wakati wa mkutano na wananchi.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa miundombinu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila amesema barabara inayounganisha  Kijiji cha Bamba na Morogoro Manispaa ambayo haikutengenezwa  itapewa kipaumbele katika bajeti ya mwaka wa Fedha 2023/2024 kuhakikisha inakamilika ili kuondoa changamoto ya kuchelewesha wagonjwa kuwahi kupata huduma za Afya  sambamba na watoto wa shule kuwahi shuleni.

Nao wanufaika wa Mradi huo akiwemo Bi. Habiba Abedi wa Kijiji cha Bamba ameushukuru uongozi wa mradi huo kwa kuwasaidia wananchi kwani umebadilisha maisha ya wanufaika kwa kuwawezesha kununua mifugo kama vile mbuzi, kuku, ng'ombe n.k. pamoja na kununua sare za watoto.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano.

Hivyo, wananchi hao wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa na Viongozi wanaouendeleza vema mradi huo na kuwafikia wananchi wa hali ya chini.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianza kutekeleza mradi wa Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) kuanzia mwaka 2000, ikiwa na lengo la kunusuru kaya masikini hapa nchini.

Bw. Jacob Kayange kwa niaba ya Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.